Zinazobamba

TIRDO YAKABIDHI MASHINE YA KUONDOA GANDA LAINI LA KOROSHO KWA CAMARTEC.

   Mkurugenzi Mkuu wa TIRDO Prof.Mkumbukwa Madundo Mtambo(Kulia Mwenye suti ya         bluu)akisainishana Mkataba wa Makabidhiano ya Mashine ya Kuondoa Ganda laini la Korosho na Mkurugezi wa CARMATEC Pythias Mtella(Kushoto mwenye shati nyekundu)

Na Mussa Augustine.

Shirika la Utafiti wa Maendeleo ya Viwanda Nchini(TIRDO) limekabidhi Mashine ya Kuondoa ganda laini la Korosho kwa Kituo cha Zana za Kilimo na Teknolojia vijijini(CAMARTEC) ili kuweza kutoa mafunzo kwa wajasiliamari katika kiwanda Darasa kilichopo Wilayani Manyoni Mkoani Singida.

Akizungumza wakati wa hafla ya  Makabidhianao hayo yaliyofanyika tarehe 29,2024 Makao Makuu ya TIRDO Jijini Dar es salaam ,Mkurugenzi Mkuu wa TIRDO, Prof.Mkumbukwa Madundo Mtambo amesema kuwa mashine hiyo imetengenezwa kwa ushirikiano na Shirika la Viwanda Vidogo Nchini (SIDO) pamoja na TEMDO ikiwa ni utekelezaji wa ombi la CAMARTEC.

Prof.Mtambo amesema kwamba mashine hiyo itasaidia kutoa mafunzo kwa wajasiliamari wanaojifunza namna ya kubangua korosho Wilayani Manyoni Mkoani Singida ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa adhma ya serikali kuhakikisha korosho zinaongezwa thamani.

“Leo tunakabidhiana Mashine hii ya kuondoa ganda laini la korosho kwa wenzetu CAMARTEC ili waweze kutoa mafunzo kwa wajasiliamari waliopo katika kiwanda darasa cha kubangua korosho Wilayani Manyoni Mkoani Singida”amesema Prof Mtambo

Nakuongeza kuwa”Naomba nitumie fursa hii kumpongeza Rais Dkt Samia Suluhu Hassani kwa kuzipatia fedha taasisi mbalimbali kwa ajili ya kuzisaidia taasisi hizo kujiendesha na kutatua changamoto zinazojitokeza ili kufikia malengo yake.

Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi Mkuu CAMARTEC ,Pythias Mtella amesema kwamba Ubanguaji wa korosho katika kiwanda Darasa umeanza mwezi Machi,nakwamba kwa sasa wanakabiliwa na chanagamo ya ukosefu wa mashine ya kuondoa ganda laini la korosho hivyo kupatikana kwa mashine hiyo itasaidia kufanya kazi yao kwa ufanisi.

Aidha amesema kuwa pamoja na kupatikana kwa Mashine ya Uondoaji wa ganda laini la Korosho bado kuna changamoto iliyobaki ya kupata mashine ya kupaki korosho kwa ajili ya kwenda sokoni.

“Lengo la serikali ifikapo mwaka 2025/26 asilimia 60 ya korosho ibanguliwe hapa nchini ,nakwamba ifikapo 2030 korosho zote ziweze kubanguliwa hapa nchini,hivyo kwa sasa inahitajika mafunzo ya kuzalisha wajasiliamari wengi wenye ujuzi  wa kuongeza mnyroro wa thamani kwa zao hilo ili kufikia malengo hayo.

Nae Mhandisi Idara ya Maendeleo kutoka TIRDO,  Mh.Atupele Kilindu amesema kwamba mashine hiyo ya kuondoa ganda laini la korosho inauwezo  wa kuondoa ganda kwa kilo 350 kwa saa nakwamba imegharimu kiasi cha shilingi milio 40 kukamilika kwake.

Hakuna maoni