Zinazobamba

Viongozi mbalimbali wa kada ya Elimu wajitokeza katika Hafla ya Kumuaga Afisa Elimu, Mkoa wa Dar es salaam Alhaj Maulid

Na, Vicent Macha DSM.

Wakuu wa shule, Maafisa Elimu pamoja na Wadau wote wa kada ya Elimu wametakiwa kumpa ushirikiano Afisa Elimu mpya wa Mkoa wa Dar es salaam Bw. Gifty Kyando ili kuweza kutimiza maono ya Rais Dkt. Samia katika kukuza na kuendeleza elimu nchini.

Hayo yameelezwa na aliyekuwa Afisa Elimu wa Mkoa wa Dar es salaam ambae sasa ni Mkurugenzi wa Idara ya Elimu msingi, Wizara ya Elimu Sayansi na Teknolojia Bw. Alhaj Maulid katika tafrija maalum ya kumuaga iliyofanyika Mbezi Beach, Dar es salaam.

Katika hafla hiyo iliyoudhuriwa na Wakuu wa shule, Walimu wakuu, Maafisa Elimu kata na Wilaya, Watumishi wa Afisa Elimu Mkoa wa Dar es salaam na wadau mbalimbali wa kada Elimu.

Mkurugenzi Maulid amewaasa walimu na Viongozi mbalimbali waliyopo katika kada hiyo kuwa ni watu wa kupenda kusikiliza kuliko kuongea. "Napenda kuwaasa Walimu wenzangu asilimia 80 muwe mnasikiliza na asilimia 20 pekee ndio muwe mnaongea, mpende kuwakiliza wateja wenu kwani wao ndio sababu ya nyinyi kuwepo hapo mlipo" alisema Maulid

Ameongeza kwa kusema kuwa anawapongeza walimu wote kwa kumuheshimisha kwa kufanya vizuri kitika mitihani mbalimbali na kuufanya mkoa wa Dar es salaam kuendelea kuwa juu kielimu.

Na mwisho amewashukuru kwa ushirikiano wao waliompa kwa kipindi chote alichokuwa katika mkoa huu wa Dar es salaam na kuwaomba waendelee kushirikiana vema na Afisa Elimu mpya Bw. Gifty Kyando ili kuendelea kuilinda heshima iliyopo, lakini pia kuendelea kumuheshimisha Afisa Elimu huyo aliyekuja kuziba nafasi yake.

Kwa upande wake Afisa Elimu wa sasa wa Mkoa wa Dar es salaam Bw. Gifty Kyando ameendelea kuwaomba walimu na watumishi mbalimbali wa mkoa huo kuweza kuwa na umoja na ushirikiano ili kuendeleza mazuri yaliyopo Dar es salaam.

Afisa Elimu huyo ameongeza kwa kusema kuwa wana Dar es salaam wamempa deni. 

"Wana Dar es salaam mmenipa deni nami sina budi kulilipa, nitahakikisha nitalilipa kwa maana kwa hiki mlichonipatia itakuwa sehemu ya kumbukumbu kwangu ya kwamba nadaiwa na njia za kulilipa ni kwa kuwaombea pamoja na kufanya kazi kwa bidii" Alisema Kyando

Aidha ameendelea kusisitiza kuwa Dar es salaam ni kipimo cha mikoa yote Tanzania kwa wengine wote wanajipima kwetu kuona wamefanikiwa kwa kiwango gani hivyo tupige kazi ili kuendelea kuheshimisha mkoa huu ambao ndio dira ya mikoa mingine, lakini pia kuheshimisha nchi na kiongozi wetu Dkt. Rais Samia

Mkurugenzi wa Idara ya Elimu msingi, Wizara ya Elimu Sayansi na Teknolojia Bw. Alhaj Maulid akiongea na Wakuu wa Shule, Walimu wakuu pamoja na Maafisa Elimu Kata na Wilaya wa Mkoa wa Dar es salaam, katika hafla ya Kumuaga rasmi kama Afisa Elimu Mkoa wa Dar es salaam.
 Kamati ya maandalizi wakipokea zawadi ya keki katika hafla ya Kumuaga rasmi Afisa Elimu Mkoa wa Dar es salaam Bw. Alhaj Maulid.
Afisa Elimu wa mpya wa Mkoa wa Dar es salaam Bw. Gifty Kyando akiongea na Wakuu wa Shule, Walimu wakuu pamoja na Maafisa Elimu Kata na Wilaya wa Mkoa wa Dar es salaam, katika hafla ya Kumuaga rasmi aliyekuwa Afisa Elimu Mkoa wa Dar es salaam Bw. Alhaj Maulid.
Baadhi ya wanakamati ya maandalizi wakimkabidhi zawadi ya keki Afisa Elimu wa sasa wa Mkoa wa Dar es salaam Bw. Gifty Kyando ishara ya kumkaribisha rasmi Mkoa wa Dar es salaam.
Afisa Elimu Kata ya Temeke akitoa neno katika hafla ya Kumuaga Afisa Elimu Mkoa wa Dar es salaam Bw. Alhaji Maulid ambaye sasa ni Mkurugenzi wa Idara ya Elimu msingi, Wizara ya Elimu Sayansi na Teknolojia.
Mwenyekiti wa Kamati ya maandalizi ya Tafrija ya Kumuaga Afisa Elimu wa Mkoa wa Dar es salaam na kumkaribisha Afisa Elimu mpya akiteta jambo na Maafisa hao.
Baadhi ya wageni walioudhuria katika hafla ya Kumuaga Afisa Elimu Mkoa wa Dar es salaam Bw. Alhaji Maulid ambaye sasa ni Mkurugenzi wa Idara ya Elimu msingi, Wizara ya Elimu Sayansi na Teknolojia.

Hakuna maoni