Na Mussa Augustine.
Ujumbe kutoka Bohari ya Dawa ya Sierra Leone umewasili Nchini Tanzania kwa ajili ya kujifunza
namna ya kuboresha mifumo ya utoaji wa huduma ya dawa kutoka kwa Bohari ya Dawa ya Tanzania (MSD) ambayo imepata mafanikio makubwa katika Nchi za Afrika Mashariki.
Akizungumza aprili 29 ,2024 mara
baada ya Ujumbe huo kuwasili nakufanya mazungumzo na Menejimenti ya MSD,Mkurugenzi wa huduma za dawa na Mfamasia Mkuu wa Serikali,Daud Msasi amesema kuwa Bohari ya Dawa ya Seirra Leone na Bohari ya Dawa nchini
Tanzania ( MSD) kupitia ushirikiano huo utaleta tija ya ushirikiano na utaongeza
fursa ya kibiashara kwa kuendelea kujinadi bidhaa wanazozalisha katika sekta ya
Dawa .
Sanjari na hayo amebainisha kuwa
Seirra Leone imeichagua Tanzania kua kituo cha kujifunzia mifumo ya utoaji wa
huduma ya dawa kwa wananchi wake kutokana na mageuzi makubwa yaliyofanywa
serikali ya Tanzania katika Sekta ya Dawa baada ya kuanzisha kampuni tanzu ya
utengenezaji na uagizaji wa dawa,Vifaa tiba na Vitendanishi kwa
kushirikiana na wadau mbalimbali ikiwemo Global Fund, UNFPA
"Andiko lao wamepeleka nchi
nyingi za Afrika na walipokaa na kuanza kuchambua ni nchi , wamegundua Tanzania
ni Nchi nzuri kwa kujifunzia kupitia MSD, sasa tutawapa ushirikiano kwani
wanataka kujifunza namna ya mifumo ya utoaji wa huduma kwa wananchi wa bara la
afrika kwa ujumla" amesema
Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa
MSD Maverre Tukai amebainisha kuwa Sierra Leone wameamka upya mara
baada ya kuvunjavunja MSD yao kutokana na machafuko ya vita vya wenyewe
kwa wenyewe hivyo wana miaka sita na wanataka waendeshe huduma kwa kasi
hivyo wmekuja kujifunza kwani sisi kuna vitu vingi tunafanana ikiwemo
manunuzi, hivyo wamevutiwa sana na uhimivu ,matumizi ya tehama, kununua bidhaa
kwa niaba ya wafadhi kwa kweli wamefurahi sanaa kuona namna MSD inavyofanya
kazi.
" Tanzania tuko vizuri
wametuomba tushirikiane sana kubadilishana uzoefu baina ya wataalam wetu na
wataalamu wao ili wafahamu vitu vingi zaidi ikiwemo kampuni tanzu ambayo kwao
haipo nasisi tutajitahidi kuwa karibu nao kwani tunashabiiana baadhi ya mifumo
ya wizara ya afya" amesema Maverre
Nae Mkurugenzi wa
huduma za Dawa na Mfamasia Mkuu Serra Leone Moses Batema amesema baada ya
nchi hiyo kukumbwa na machafuko ya vita vya wenyewe kwa wenyewe ilipelekea
taasisi nyingi za nchi hiyo kuvunjika ikiwemo Bohari ya Dawa ya nchi hivyo
kwasasa imeanzishwa upya ambapo mpaka sasa ina miaka sita tangu kuanzishwa
kwake na nia yao ni kuiendesha vizuri isiyumbeyumbe kiuendeshaji iwe imara kama
MSD ya Tanzania.
"Tumekuja Tanzania kujifunza namna MSD inavyojiendesha bila kutetereka kifedha,
kiutendaji,tumejionea na kujifunza ubunifu mkubwa unaofanywa na wenzetu( MSD)
hivyo tutashirikiana kwa ukaribu zaidi kupitia wataalamu wetu kwa kufundisha
ujuzi wa mifumo mbalimbali ikiwemo ununuzi na usambazaji wa dawa, na vifaa
tiba" amesema Dkt Katema.
Halikadhalika Kaimu Naibu Mkurugenzi Mkuu na Mkurugenzi wa Uendeshaji Bohari ya
Dawa ya Sierra Leone Jatu Abdulai ameishukuru menejiment ya MSD kwa kuonesha
ushirikiano mzuri huku akiwa na matumaini makubwa ya Bohari ya Dawa ya nchi
yake kupata mafanikiao makubwa kupitia ushirikiano huo.
Hakuna maoni
Chapisha Maoni