Zinazobamba

Halotel yatoa Msaada wa Chakula na Vifaa vya Nyumbani kwa wanawake wenye Mahitaji Maalumu Mtwara.

lotel ikiwa ni kampuni ya mawasiliano Tanzania, ikitoa huduma mbalimbali za mawasiliano na ikiendelea kukidhi mahitaji ya wateja wao. Kwa kuzingatia usalama na uaminifu Halotelinaendelea kutoa huduma bora na kuleta mabadiliko chanya katika sekta ya mawasiliano na jamii kiujumla.

Katika kuhadhimisha mwezi wa kumsheherekea Mwanamke na kukaribisha sikuukuu za Pasaka, Halotel Tanzania yatoa msaada kwa wanawake chini ya Taasisi ya ‘Jukwaa la wanawake na wasichana wenye ulemavu Mtwara’ kusaidia changamoto mbalimbali wanazozipata wanawake hao.

Akiongea katika tukio hilo Mkurugenzi wa Halotel tawi la Mtwara Bwana Emmanuel Monyo “Halotel inaendelea kusimama imara katika kufanikisha malengo yake ya kukuza usawa na ujumuishaji katika pande zote za jamii.

 Lakini kwa kuwasaidia wanawake hawa Mtwara Halotel inaonyesha dhamira yake ya kuleta mabadiliko katika jamii na kuunda ulimwengu weye uwezekano na fursa kwa wote”.

Afisa uhusiano na mawasiliano wa Halotel, Roxana Kadio ambae aliwasilisha msaada huo alisema Halotel inaedelea kujenga ujumuishaji ambao kila mtu bila kujali uwezo wao anaweza kushiriki kikamilifu katika jamii, aliendelea kusema kuwa Halotel iliamua kuwaunga mkono wanawake wa Mtwara baada ya kujifunza kuwa wanapitia changamoto za chakula na vifaa vya nyumbani na kama kampuni inayokua nia yetu kutoa mkono wa msaada kwa jamii ya kitanzania.

“Mahitaji yaliyotolewa na Halotel ni pamoja na Chakula kama Mchele, Sukari na Mafuta ya kupikia lakini pia kutoa msaada wa magodoro na vifaa vingine vya nyumbani. Vyote hivi ni katika kuwahudumia wanawake hawa na kuwaonesha kuwa hawako peke yao katika changamoto wanazozipita” Roxana alisema.

 Aliendelea kusema kuwa msaada huu pia unalenga katika kuwatoa upweke wanawake hawa katika mahitaji yao. Na kwamba Halotel haitoishia kusaidia tu wanawake na wako kwenye mpango wa kukuza uhitaji wa jamii kiujumla.

Halotel itaendelea kutoa ushirikiano kwa majukwaa ambayo yanajikita katika kuwainua wanawake. Lakini pia Halotel itaendelea kutia chachu ya maendeleo kwa wateja wake na jamii kiujumla.




Hakuna maoni