Zinazobamba

TANZANIA NA HUNGARY ZASAINI MKATABA WA KUSHIRIKIANA SEKTA YA MAJI NA USAFIRI WA ANGA


NA Mussa Augustine.

 Tanzania  na Hungary zimetiliana saini Mikataba ya  kushirikiana katika Masuala ya Maji na Usafiri wa Anga nakwamba  Hungary iko Mbioni kufungua ubalozi wake hapa nchini.

 Akizungumza  leo Machi 24,2024  jijini Dar es Salaam Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki,Mh. Januari Makamba amesema kuwa hatua hiyo inatokana na Rais wa Hungary kuja Nchini Tanzania Mwaka 2023,nakusababisha muendelezo wa ushirikiano wa muda mrefu uliopo baina ya Nchizo.

 "Tumepata ugeni kutoka Hungary na hii inakuja baada ya Rais wao kuja hapa Tanzania mwaka jana na kusababisha kuendeleza ushirikiano wa muda mrefu uliopo baina ya nchini zetu mbili," amesema Mh.Makamba .

 Aidha ameongeza kuwa  Mazungumzo hayo baina yake na ujumbe kutoka  Hungary ulioongozwa na Waziri wa Mambo ya Nje  wa taifa hilo, Peter Szijjàrtò wamekubaliana mambo kushirikiana mambo mbalimbali ikiwemo kuanzisha safari za anga ya moja kwa moja hadi hapa nchini.

 Waziri Makamba amefafanua kuwa safari za anga ya moja kwa moja kutoka Hungary kuja Tanzania itasaidia kutanua wigo  wa kibiashara baina ya mataifa hayo mawili.

 “Hatua hii pia itaongeza watalii wanaotoka Hungary kuja Tanzania ambapo kwa miaka miwili iliyopita watalii 5000 waliingia hapa nchini kutoka katika nchi hiyo na mwaka jana waliongezeka na kufikia 11,000,sasa tutakua katika hatua nzuri zaidi” Amesisitiza Waziri Makamba

 Aidha amesema kuwa ongezeko hilo la watalii wanaotoka Hungary kuja Tanzania litaongezeka pindi itakapoanzishwa safari ya anga ya Moja kwa Moja hali ambayo itasaidia  kufungua fursa nyingi za kibiashara.

 Aidha katika sekta ya  kibiashara Nchi hizo zimekubaliana  kwa pamoja  kuandaa amakongamano ya sekta binafsi yatakayofanyika  Hungary na Tanzania.

 Pia wamekubaliana kuendeleza  ushiriano kwenye elimu na kuongeza scholarship kwa Watanzania kwenda kusoma Hungary na Tanzania itakuwa ikitoa nafasi tano kwa vijana wa nchi hiyo kuja kusoma hapa nchini katika vyuo mbalimbali vilivyopo kila mwaka.

 "Hadi sasa tayari wanafunzi 146 wa kitanzania wamepata fursa ya kusoma nchini Hungary na kila mwaka tunapeleka vijana wetu kusoma huko na hiyo imekuja baada ya wenzetu mwaka 2018 kuanzisha programu ya Scholarship   amesema.

 Amesema kuwa sababu ya kuchukua hatua ya Kusaini mkataba wa kushirikiana katika Sekta ya Maji  ni kutokana na taifa hilo kuwa kuongoza katika teknolojia ya kudhibiti mafuliko, maji taka na ya kutumia.

 “Maarifa yao Makubwa katika sekta ya maji ndio imetuvutia kusaini mkataba unaohusu masuala hayo ili nasi tupate utaalamu wa kutosha katika nyanja hiyo, amesema Waziri Makamba mbele ya Waandishi wa habari

 Naye Waziri wa Mambo ya Nje wa Hungary, Peter Szijjàrtò amesema kusaini Mkataba wa  usafri wa anga utasaidia kuendeleza ushirikiano uliopo baina ya mataifa hayo mawili,nakwamba mikataba hiyo itatekelezwa kama walivyokubaliana.


Hakuna maoni