Zinazobamba

Sheikh Othman Michaela: hatutafunga huduma zetu, wananchi watoe hofu

 



 




Mtalaamu wa kueneza da’aawa kwa umma kupitia kitabu kitukufu cha Quran na suna za Bw. Mtume Muhammad (saw) Sheikh Othmani Michael amewatoa hofu waislamu na wasio kuwa waislamu kuwa huduma zake zitaendelea kupatikana kama kawaida na kwamba kilichotokea ni sehehmu katika changamoto za kazi.

 

Alisema anaamini kazi anyoifanya ni muhimu, hivyo ataendelea nayo kama kawaida kwani huo ni  wito ambao analazimika kuufanyia kazi ili watu wapate kunufaika.

 

Akizungumza katika mahojiano maalum na mtandao wa fullhabari blog, ofisini kwake Sheikh alisema mpaka ofisi yake imepokea kazi nyingi kutoka kwa wananchi ambao wanahitaji huduma, hivyo hawana mpango wa kufunga huduma zao.

 

Sheikh Othman ambaye pia ni tabibu wa da’aawa za kisunna ameongeza kusema kuwa kupitia ofisi yake waislamu na wasio waislamu waliweza kutatuliwa changamoto zao na faida nyingi imepatikana ikiwamo watu wengine kuiga anachokifanya.


“Kupitia mitandao ninayoiongoza watu wengi wamepata kufaidika, mpaka sasa nchi zingine zimeiga utaratibu niofanya, kuna watu wameanzisha maudhi ya papo kwa papo (live progammes), wengine wanafanya ya kurekodi (recording), hivyo tutaendelea na kazi hiyo,” alisema.

Mimi tamaa yangu ni kuona nasuluhisha matatizo mengi kwa kadri ya uwezo wangu, natamani siku moja nikikutana na Allah niwe nimesuluhisha kesi bilioni moja, na nikiulizwa niwe na cha kujibu

Hivi karibuni Baraza kuu la waislamu mkoa wa Dar es salaam limemuita na kufanya mazungumzo na Sheikh Othmani kwa lengo la kujua sababu za kusambaza video ambayo imeleta sintofahamu.

 

Sheikh alisambaza video katika mitandao ya kijamii akifanya mahojiano na wanawake wawili, binti na mama mzazi waliokwenda ofisini kwake kupata suluhu ya changamoto waliyoipata.

Katika kikao hicho Baraza la masheikh wa mkoa limebaini kuwa kilichokuwa kinasambaa mitandaoni hakikuwa na ukweli wowote bali ni igizo la kisa cha kweli kilichotokea huko nyuma.

Sheikh Alhad Musa Salum alitumia cheo chake kuwaomba waislamu kokote nchini kumdhania kheri Sheikh Othmani Michael kwani baraza lake limebaini kuwa hakuwa na nia mbaya katika kutengeneza video hiyo.

 

Sheikh Othmani aliwahi kusuluhisha kisa kama hicho, kutokana na uzito wa kisa chenyewe, busara ilimuongoza kucheza kisa hicho kwa lengo la kufikisha daawa kwa umma, bahati mbaya watu wameipokea tofauti.

Aidha alibainisha kuwa  Bakwata haiwakatazi Masheikh, maimam, maostazi kushughulikia migogoro ya waislamu sababu baraza lenyewe linaanzia huko ngazi ya jamii.

Aidha Sheikh Alhadi alimsifu Sheikh Othman Michael kwa kazi kubwa anayoifanya ya daawa na kusisitiza kuwa wao kama walezi wanamuunga mkono kwa kazi hiyo ya kuitengeneza jamii, amewaomba waislamu kumchukulia udhuru kwa tukio hili kwani nia yake ilikuwa ni njema ya kufikisha ujumbe.

Aidha amekosoa tabia ya waislamu kukosoana kupitia vyombo vya habari huku akishauri njia nzuri ya kukosoa ni kutafutana na kujua ukweli kisa kuchukua hatua stahiki.

 

 


No comments