Zinazobamba

Ukeketaji bado ni tatizo kubwa Tanzania, wadau washauliwa kuvunja ukimya

 



Na mwandishi wetu





Mkurugenzi wa Jukwaa la utu wa mtoto (CDF) Koshuma Mtengeti amewashauri viongozi wa dini, serikali na wadau wengine hapa nchini kukemea vitendo vya ukeketaji kwani tatizo hilo bado lipo na linachangia katika unyanyasaji wa kijinsia

Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake, Mtaalamu huyo wa masuala ya utetezi wa mtoto, amekili kuwa licha ya jitihada ambazo zinachukuliwa kunahitajika nguvu ya pamoja ili kuodnoa tatizo hilo.

 

Alisema Pamoja na jitihada ambazo serikali imekuwa ikizichukua bado kuna baadhi ya mikoa waifanya kazi ya ukeketaji kama sehehmu ya kuleta kipato lakini pia wanasiasa wamekuwa wakichangia kurejesha nyuma nguvu ya kupambana na wakeketaji.

“Unajua kwa baadhi ya makabila hili suala wamelifanya ni sehehmu ya kujipatia kipato, lakini pia kuna wanasiasa ambao wanasema hadharani kuwa hawa ni wapiga kura wangu waacheni watekeleze mila, sasa hapo bado kuna shida,” alisema.

Aidha Koshuma ameshauri serikali kuwekeza elimu katika kuwawezesha wananchi kiuchumi hasa maeneno ambayo yanaongoza katika zoezi la ukeketaji, dhamira ikiwa ni kuwavutia watu waachane na ukeketaji na wafanye kazi halali.

 

Koshuma ambaye ameyazungumza hayo wakati alipotakiwa kutoa tathmini yake juu ya ukeketaji Tanzania,

 

Tukiwa tunaelekea siku ya kupinga vitendo vya ukeketaji duniani  lazima tujitakali, tumefanikiwa kiasi gani, ukweli tumefanikiwa lakini bado tunayo kazi ya kufanya.

 

Alisema takwimu za shirika la afya duniani zinaonyesha kuwa vitendo hivyo vimepungua kutoka asilimia 18 mwaka 1996 hadi asilimia 10 mwaka 2016

 

Alisema mafanikio hayo yamepatikana kutokana na ushirikiano na jitihada kati ya serikali na Asasi za kiraia pamoja na wadau wengine wa serikali kupinga ukeketaji na kujikita zaidi katika kutoa elimu ya kubadili mitizamo ya jamii juu ya mtoto wa kike.

 

 

Amezitaja baadhi ya sababu ambazo zimekuwa zikitajwa kuendelea kwa vitendo ivyo ni pamoja na njia ya kuonyesha kuwa msichana amekuwa mwanamke kamili na tayali kuweza kubeba majukumu ya kifamilia pamoja na kujiongezea kipato kwa wanaofanya kazi hiyo (angariba).

 

Mikoa ambayo imekithiri kwa vitendo vya ukeketaji ni pamoja na Manyara ambayo inaongoza kwa kuwa na asilimia 58, Dodoma asilimia 47, Arusha asilimia 41 na Mara asilimia 32.


No comments