Zinazobamba

NEEC, GGML kukutana na wajasiliamali na watoa huduma 150 mkoani Geita

 




Issack Tadheo, Dar es salaam

Baraza la uwezeshaji wananchi kiuchumi kwa kushirikiana na Mgodi wa dhahabu wa Geita (GGML) wameandaa mafunzo kwa vitendo kwa  kwa wajasiliamali na watoa huduma 150 ambayo atafanyika katika ofisi ya sido mkoani Geita.

Mafunzo kwa wajasiliamali na  watoa huduma yanatarajiwa kuanza machi, 8 2021 na kukamilika kwake mach 19, 2021 na yatahusisha stadi mbalimbali ikiwamo usindikaji wa vyakula, utengenezaji wa sabuni, chaki, mabegi, na urembo wa wanawake.

Akizungumza na Fullhabari Blog, katibu mtendaji wa Baraza la taifa la uwezeshaji wananchi kiuchui, Bibi Beng’I Issa amesema hiyo ni fursa kwa wakazi na wafanya biashara wa mkoa wa geita kujitokeza katika mafunzo hayo kwani ni muhimu sana kwa kazi zao.

 

Lengo la mafunzo ni kuwawezesha washiriki kuboresha bidhaa zao ili zikizi viwango vya  soko pamoja na kupata alama za ubora kutoka mamlaka ya viwango Tanzania  pamoja na kupata  alama za utambuzi  wa bidhaa zao kutoka GSI

Pogram hii itatekelezwa kwa kipindi cha Mwaka mmoja nakunufaisha wajasilliamali zaidi ya 300 (Miatatu), ikiwemo mpaka sasa pogramu hii imewezesha mafunzo ya usimaminzi wa biashara na ushindani katika zabuni kwa wajaliamali wapatao 365 katika mafunzo ya awamu ya kwanza,

 Pia katika mafunzo ya awamu ya pili watoa huduma 148 (Miamoja arubaini nanane) watapatiwa Elimu na Mbinu za Kujiunga Katika Kongamano    

Ili kuwaongezea ujuzi na nguvu za kushindana vema ktk soko la pamoja, Aidha katika kutekeleza pogramu hii baraza kwa kushirikiana na Mgodi wa Dhahabu wa Geita wameandaa mafunzo kwa vitendo kwa wajaslliamali na watoa Huduma 150 (Miamoja hamsin) ambayo yatafanyika mkoan geita Ambayo yatahusisha Stadi mbalimbali kama vile usindikaji wa vyakula utengenezaji wa sabuni na batiki,ushonaji, kudarizi, utengenezaji chaki, mifuko mbadala, mabegi na urembo wa wanawake, ufugagi kuku na kilimo cha bustani, lengo la mafunzo haya nikuwawezesha kutengeneza nakuboresha bidhaa zao ili zikidhi viwango vya soko la pamoja ili ziweze kutambuliwa na mamlaka ya viwango nchini (TBS)

 


No comments