HUYU NDIYE MWENYEKITI WA CHADEMA ALIPIGWA NA WAFUASI WA CHADEMA WAKIMTUHUMU KUSHILIKIANA NA ZITTO KABWE KUKILARUA CHAMA
Mwenyekiti wa chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) wilaya ya Temeke Joseph Yona amepigwa na watu wasiojulikana na kisha kutupwa kwenye eneo la Ununio kwenye Magorofa ya Wasomali Kawe Dar es salaam.

Shuhuda Abdul Ally ambae ni mkuu wa nyumba zilizokaribu na alikopigwa Mwenyekiti huyu, anasema walisikia kelele za huyu mtu kupigwa saa tisa usiku na walipomsogelea walimkuta peke yake.
‘Niliomba wasiniue, wamenipiga sana… wamenichukua saa tano nyumbani kwangu Kwa Aziz Ally, wao walikua na gari kama ya Polisi lakini inaonekana sio ya polisi wakasema tunakupeleka Central, tulikua wanne na hawakuhangaika na mtu wakanichukua mimi moja kwa moja.. tulipopanda kwenye gari wakachukua nguo yangu wakanifunga uso, wakaanza kunipiga wakisema nisiwajibu na hawakuniambia chochote’
Unaweza kusikiliza maelezo yake mengine akihojiwa kwa kubonyeza play hapa chini..
Hapa mwandishi wa blog hii Ndg. Vicent Karoli anashuka nayo......
CHAMA cha
Demokrasia na Maendeleo Chadema kimeingia kwenye kashfa nzito baada ya
kuhusishwa kwenye utekaji wa Mwenyekiti wa Chadema wilaya ya Temeke Ndg Joseph Yona.
Taarifa
toka ndani ya jeshi la polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam ambapo mwandishi wa
mtandao huu amezipata baada ya kuthibitishwa na Kamisha wa kanda Maalum ya Dar
es Salaam Suleiman Kova Mbele ya Waandishi wa Habari leo Zinasema
Jeshi hilo la polisi linafanyia uchunguzi wa kina kuhusu tukio la kutekwa nyara
,kupigwa na kujeruhiwa na hatimaye kutupwa vichakani dhidi ya mtu anaitwa Joseph Yona miaka 32 mkazi wa
Temeke mtoni kwa Azizi Ally.
Taarifa hiyo inasema alitekwa na kutupwa vichakani ni mwenyekiti wa chadema wilaya ya Temeke ambaye pia ni Mtaalam wa
Maabara chuo cha Elimu (DUCE) kilichopo Changombe.
Vilevile taarifa hiyo inafafanua mnamo tarehe 7 mwezi huu saa 5 usiku eneo la
Ununio ,Bw.Joseph Yonna alienda kuaomba msaada
kwa mlinzi wa kampuni binafsi aitwaye Ismail Swalehe ili aende kituo cha
polisi kuripoti baada ya kupigwa na watu sita na kumtupa huko kichakani
Ndipo milinzi huyo alikubali na kumpeleka kwa mwenyekiti wa
serikali ya mtaa wa Ununio,ndipo mwenyekiti huyo ndipo alipowasiliana na mkuu wa
polisi kawe ambaye alifika eneo la tukio
hilo akifuatana na Rpc wa kinondoni Acp Camilius Wambura.
Maofisa wa
Polisi walimuhoji Joseph Yonna Kuhusu Majeraha aliyonayo usoni sehemu
mbalimbali za mwili wake.
Ndipo mlalamikajia aliweza kujieleza kuwa yeye ni mkazi wa kwa
Azizi Ally wilaya ya Temeke na kwamba ilpofika saa 5.Kamili usiki ya tarehe 6
mwezi huu alikuwa akipata kinywaji katika Grocery ya Mgumbini akiwa na wenzake
watatu walikuwa wakimalizia Vinywaji.
Ghafla walitokea watu sita ambao walimtaka
aende nao walijitambulisha kuwa wao ni maofisa wa Polisi katika kituo cha kati.
Ndipo katika watu hao sita aliweza kumtambua mtu
mmoja kuwa ni mwanachama mwenzake wa chadema na alipojalibu kuulizia kuhusu
huyo mtu walimwingiza ndani ya Gari aina
Land Cruiser na kufunga kitambaa usoni na kuondoka naye.
Katika hatua
nyingine mlalamikaji alizidi kusema waliomteka walianza kumhoji ni kwa nini
anaendelea kumshabikia Zitto Kabwe wakati ni
mtu anayeharibu chama chao yaani chadema.pili walimtaka akawaonyeshe rafiki yake ambaye
anajulikana kwa jina Habibu
Mchange.ndipo walizidi kumpiga mpka wakampelekea majeraha kwenye jicho na
kichwani.
Uchunguzi wa
awali unaonyesha wazi kuwa tukio hili lina uhusiano wa moja kwa moja na mgogoro
unaoendelea katika chama cha siasa cha chadema juu ya Zitto kabwe na
wenzake.Aidha kabla ya tukio hili,mlalamikaji alikuwa anapokea simu nyingi za
vitisho kutoka kwa viongozi wa ngazi
mbalimbali wa Chadema ambao anadai
anawafahamu.
Vilevile
Taharifa hiyo inasema Jeshi la polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limeanza uchunguzi wa sakata hilo
Uchunguzi wa
mwandishi wa mtandao huu umebaini nkuwa Habibu Mchange ni miongoni mwa watu
wanaosakwa sana na wanasiasa kutokana na kuhusika katika mipango ya kukihujumu
chama hicho.
Wachambuzi
wa masuala ya mambo ya kisiasa waliozungumza na mtandao huu wanasema siasa za
Tanzania zimekuwa hazistawi kutokana na wanasiasa wa vyama vikuu vya upinzani kuwa na tamaa za pesa na
kujionyesha kuwa wanashabikia upande mmoja wasiasa
No comments
Post a Comment