Zinazobamba

TCRA YAWAONYA WANAOSAMBAZA PICHA ZA MAREHEMU,SOMA HAPO KUJUA

NA KAROLI VINSENT
MAMLAKA ya Mawasiliano nchini (TCRA) imewataka watanzania kuacha tabia ya kuweka picha mitandaoni za watu waliokufa au picha za ngonokwa  kuwa  vitendo hivyo ni kosa la jinai.
Pia Mamlaka hiyo imetaka jamii kutumia mitandao ya kijamii kama njia bora ya kujiletea maendeleo .

Hayo yamesemwa leo Jijini Dar es Salaam na Mkurugenzi mkuu wa (TCRA) Mhandisi James Kilaba wakati wa ufunguzi wa semnina ya kutoa elimu kwa viongozi wa mkoa wa Dar es Salaam ili waweze kutumia mitandao ya kijamii kwa manufaa ya nchi.

Mhandisi Kalaba amesema kwa sasa  watu wamekuwa wakitumia mitandao ya kijamii kwa kuweka  picha ambazo hasistahili kwa jamii.

“Leo kwa mfano ikitokea ajali ambao watu wamekufa au kupata ajali  unakuta mtu anachukua picha hizo na kuziweka kwenye mitandao ,nataka kuwambia hili ni kosa la jinai”amesema Mhandisi Kalaba.

Amesema kwa sasa jamii haina budi kubadilika na kuanza kutumia mitandao kama njia ya kujiletea kipato .

“Jamii inatakiwa kutumia mitandao ya kijamii kama njia ya kujiletea kipato,kwa mfano kwa sasa tumeanzisha anauni za makazi ambazo hizi zitaisadia serikali kuwafahamu na kuweza kurahisisha mipango ya kimaendeleo’amesema Mhandisi huyo.