Zinazobamba

MAENDELEO BANK PLC YAKUZA MTAJI WAKE NA KUFIKIA BILION 19,YAJIPANGA KUTOA HUDUMA NCHI NZIMA.

 

Na Mussa Augustine.

Mkurugenzi wa Maendeleo  Benki Plc’ Dkt. Ibrahim Mwangaraba amesema kuwa kuwa Benki hiyo imeendelea kukua mwaka hadi mwaka ambapo kwa Mwaka 2023 matokeo ya kifedha yameonesha kukua kwa faida ya asilimia 66% baada ya kodi na kufanya faida baada ya kodi kuongezeka hadi shilingi Bilioni 2.3 kutoka shilingi Bilioni 1.4 Mwaka 2022.

 Hayo ameyasema  leo April 17/2024 wakati akizungumza na waandishi wa habari Katika ofisi za Benki hiyo jijini Dar es Salaam wakati akitoa taarifa ya Maendeleo ya Benki hiyo kwa Mwaka 2023  nakusema kuwa Baadhi ya vichocheo vya mafanikio ya Benki hiyo ni pamoja na ukuaji wa faida baada

 Benki hiyo ambayo niya kwanza nchini kuorodheshwa katika Soko la Hisa la Dar es Salaam (DSE,) na kuweka historia ya kuwa benki yenye faida kwa miaka tisa mfululizo tangu mwaka wa pili wa kuanzishwa kwake ni pamoja na kuimarika kwa ubora wa mikopo kutoka mikopo chechefu ya asilimia 5.2 mwaka 2022 hadi kufikia asilimia 4.95 mwaka 2023 kulikosababishwa na kuimarika kwa hali uchumi na kufanya wateja wao kulipa mikopo kwa wakati.

 "Ndugu waandishi wa habari ukuaji huo wa faida  wa kuvutia umechangiwa zaidi na mikakati mizuri ambayo benki ilijiwekea kwa mwaka 2023 pamoja na usimamizi bora wa watendaji na wafanyakazi wa benki hiyo kwa kushirikiana na wateja na wadau mbalimbali." Amesema Mwangalaba.

 Dkt Mwangaraba ameendlea kusema  kuwa mali za benki zimeongezeka kwa asilimia 17% kutoka shilingi za kitanzania Bilioni 107.0 kwa mwaka 2022 hadi kufikia shilingi Bilioni 125.0 kwa mwaka 2023 huku mtaji wa benki ukiimarika kwa asilimia 12%kutoka shilingi za kitanzania Bilioni 17 kwa mwaka 2022 hadi shilingi Bilioni 19 kwa mwaka 2023.

 Akizungumzia kuhusiana mtaji na kuwafikia wananchi katika Mikoa nchini kote Dr. Mwangalaba amesema kuwa, Benki hiyo imefikisha mtaji wa Shilingi Bilioni 19 ambao unakidhi benki kufanya kazi nchini kote ili kuhakikisha wateja wake wanapata mikopo na kuendleza biashara zao bila tatizo lolote.

 “Kutokana na kuweza kukuza mtaji na kufikia bilioni 19 kunaiwezesha benk hii kufanyakazi nchi nzima hivyo tumeshaanza  mazungumzo  na Benki Kuu ya Tanzania (BOT,) ili tupate kibali cha kufungua matawi Mikoani na kuwahudumia Watanzania wengi zaidi zaidi,na mazungumzo yetu yapo katika hatua nzuri”amesema Dkt.Mwangaraba

 Nakuongeza kuwa  “kumekuwa na ongezeko la Amana za wateja kwa asilimia 15 kutoka shilingi Bilioni 78.0 mwaka 2022 hadi kufikia shilingi Bilioni 90.0 kwa mwaka 2023.

 Amesema kuwa mikopo ya wateja imeongezeka kwa asilimia 21 kutoka shilingi za kitanzania Bilioni 61.0 hadi shilingi za kitanzania Bilioni 74.0 kwa mwaka 2023,ukuaji huo utaendelea kwa kuwa Benki imejipanga kutoa huduma kwa ufanisi zaidi kwa wateja wake.

 Aidha Mkurugenzi huyo wa Mandeleo Bank Plc amefafanua kuwa utendaji kazi bora wa mwaka 2023 umejenga msingi thabiti wa utendaji kwa mwaka 2024 ambapo wamejipanga kutanua huduma zaidi kwa kufungua angalau tawi moja na kuongeza mawakala wapya zaidi ya 500 kutokana na mafanikio makubwa ya mwaka 2023 ambapo walifunga na nakuongeza mawakala 1600 katika mikoa 11 nakufanikiwa  kukusanya zaidi ya Bilioni 5 kila mwezi kama amana kila mwezi kupitia wateja wake.

 “Benki inawekeza sana katika teknolojia na kwa mwaka 2024 tumejipanga kuanzisha huduma mpya za kidigitali ikiwemo Benki mtandao yaani Internet Banking, mfumo wa ukusanyaji malipo ikiwemo ada za shule (PCS,) na mikopo kwa njia ya simu ambayo itawezesha benki kuongeza faida kwa fedha za wanahisa kwa mwaka 2024 na kuboresha njia mbadala za upatikanaji wa huduma za wateja.

 Nakuongeza kuwa "kwa kuonesha juhudi za kuboresha na kusogeza huduma kwa wateja mwaka huu 2024 tumefungua tawi jipya Mbagala hapa jijini Dar es Salaam likiwa tawi la tano huku tukiwa na lengo la kusogeza huduma zetu kwa wakazi wa Mbagala na maeneo jirani.” Amesisitiza  Dkt Mwangaraba.

 

Hakuna maoni