Zinazobamba

Filamu zaidi ya 100 kutoka nchi 33 Duniani kuonyeshwa katika Tamasha la ZIFF mwaka 2022.

 Na. Vicent Macha

Tamasha la kimataifa la filamu Zanzibar (ZIFF) mwaka 2022 limekuja na mikakati ya kuinua filamu za Kitanzania kufikia katika ubora wa kimataifa, ambapo filamu 101 zitaonyeshwa kutoka nchi 33 duniani.

Mratibu wa Tamasha la Kimataifa la Filamu Zanzibar (ZIFF) Prof. Martin Muhando.

Hayo yameelezwa na Mratibu wa Tamasha Prof. Martini Muhando wakati akiongea na waandishi wa Habari mapema jana jijini Dar es salaam.

Aidha Prof. Martin amesema kuwa filamu ambazo zinatarajiwa kuonyeshwa kwenye Tamasha la ZIFF ni kutoka katika mataifa ya Umoja wa Ulaya (EU), Tanzania, Kenya na Afrika ya kusini, ambapo itasaidia washiriki kuweza kujifunza tamaduni mbalimbali za mataifa shiriki.

Ameongeza kuwa ni jambo zuri kuona kwamba kwa nchi kama Iran ambayo ni mara ya kwanza kushiriki lakini imeweza kuleta filamu Zaidi 660, Na kwa upande wa Bara la Ulaya pia limeweza kuleta filamu 465.

Baadhi ya washiriki wakifuatilia mkutano kwa umakini.

Ameendelea kusema kuwa juni 18 mwaka huu itakuwa siku ya ufunguzi na filamu itakayokuwa ya kwanza kuonyeshwa inaitwa “Vuta Nkuvute” ambayo imevunja rekodi hapa nchi.

“Tunahisi filamu hii inayoitwa Vuta Nkuvute itatuinua kidete watanzania na ni filamu ya Afrika Mashariki, ndio maana imepata nafasi ya kuonyeshwa kwenye tamasha hili la kimataifa (ZIFF)” Amesema Prof. Martini

Ameongeza kuwa wakenya licha ya kuwa ni washindani wakubwa n ani watu wenye kuleta upinzani mkubwa kwa watanzania, lakini pia wamesaidia kuongeza msisimko na kuleta mafanikio kwenye tamasha la ZIFF na tasnia ya Filamu ya Tanzania.

Amesisitiza kuwa kwa upande wa Afrika ya kusini wamekuwa ni washirika wazuri kwa Tanzania licha ya harakati za uhuru tu lakini watu kutoka katika taifa hilo wamekuwa kipaumbele kuzindua na kuleta flamu za katika tamasha la ZIFF.

Lakini pia amewapongeza DW Academy kwani wamekuwa na mchango mkubwa sana katika tamasha hilo na kusema kuwa kwa mwaka wapili mfululizo wamekuwa wakiendesha mafunzo kwa washiriki ya namna ya kuboresha kazi zao ili ziwe na viwango vya kimataifa.

Baadhi ya wageni waliyofika katika mkutano wa waandishi wa habari kuzungumzia Tamasha la ZIFF 2022.

No comments