Bima ya Kiislam (Takaful) kuanza kutumika Mei
Hatimaye miongozo ya bima ya kiislam (TAKAFUL) iliyokuwa ikisubiliwa kwa hamu na waislam walio wengi imezinduliwa rasmi jana na kwamba sasa makampuni yanayotaka kufanya biashara hiyo yanaweza kupeleka maombi TIRA kuanzia mwezi Mei 1, 2022 ili waweze kusajiliwa tayari kwa kufanya biashara.
Akizungumza
katika hafla ya uzinduzi wa miongozo hiyo iliyofanyika katika ukumbi wa
Kimataifa wa Mwl. JK Nyerere uliopo Posta Jijini Dar es Salaam, Kamishna wa
bima kutoka mamlamka ya usimamizi wa bima Tanzania (TIRA) Dkt
Baghayo Saqware alisema miongozo hiyo
itasaidia kuwezesha wawekezaji wanaofuata misingi ya dini ya kiislam kuwekeza
katika biashara ya bima.
“Muongozo
huu utaanza kutumika Mei 1, 2022. Maana yake ni kwamba ikifika tarehe hiyo
Makampuni yanayotaka kufanya biashara ya Takaful yanaweza kuleta maombi yaweze
kusajiliwa na kuanzisha biashara. Bima ya Takaful inafuata misingi ya kisheria
(sharia compliance),” alisema Saqware
Vilevile
alisema kuzinduliwa kwa miongozo hiyo kunafungua milango kwa wananchi kuanza
kupata huduma za bima kwa kufuata misingi ya Sharia Compliance.
“Ni
mategemeo yetu kuwa sasa wananchi ambao wanahitaji huduma kutoka kwa taasisi za
namna hiyo wataanza kujiunga ili kupata kinga na kuingia kwenye mfumo rasmi wa
kifedha hapa nchini,” aliongeza.
Kwa
upande wake Mwenyekiti wa Cifca, Aref Nahd alisema kuzinduliwa kwa miongozo
hiyo ni hatua kubwa imepigwa, japo bado hawajafika katika hatua wanayo itaka.
Aidha
Mwenyekiti huyo alisema Taasisi hiyo iko tayari kufanya kazi na Taasisi yeyote
inayotaka ushauri wa Takaful, kwani wanao wataalam wa kutosha kutoa elimu hiyo.
Naye
mratibu wa CIFCA Sheikh Muhammad Issa alisema Biashara ya TAKAFUL ni kwa faida
ya watanzania wote, na ni matumaini yake kuwa mifuko itatuna Zaidi kama watu
wataifanya biashara hiyo ipasavyo.
Kwa
upande wake mratibu wa zoezi la uandaaji wa miongozo ya bima 2022, Muyenge
Zakaria amewapongeza CIFCA kwa ushirikiano walio utoa hadi kukamilika kwa
muongozo wa TAKAFUL.
Bw.
Zakaria alisema kwa kiasi kikubwa Cifca walitoa maelekezo muhimu yaliyochangia
kutengenezwa kwa muongozo huo ambayo unatarajiwa kuleta tija katika taifa.
“baada
ya uzinduzi huu tutaanza kutoa mafunzo mbalimbali, kwenye muongozo wa Takaful
tutashirikiana na CIFCA, kimsingi wawezeshaji wetu watakuwa CIFCA. Mafunzo
yataanza na wasimamizi wa sheria (Regulator) na baadae tutawaendelea wadau
wengine.
Wadau
mbalimbali walioudhuria hafla hiyo sasa wanaoona wawekezaji wataongezeka hasa
kutoka katika nchi zenye kufuata misingi ya dini tukufu ya Kiislam huku wakipanua
wigo mpana wa utoaji bima kwa makundi yote
Inaelezwa
kuwa mchakato wa takafuli ulianza toka mwaka 2014 huku kituo cha ushauri wa
mfumo wa fedha wa Kiislam CIFCA wakiwa na mchango mkubwa katika kueleza
faida za biashara ya TAKAFUL.
No comments
Post a Comment