Zinazobamba

Mufti Tanzania ataka Waislam kuacha kulalamika

 Mufti na Sheikh Mkuu wa Tanzania Sheikh Abubakari Zubeir amewataka vijana wa kiislam kuacha kulalamika kuhusu furasa za ajira na badala yake wajikite katika matayarisho ili wawe na sifa ya kuzipata zitakapotokea.

Mufti amebainisha hayo katika mashindano ya quran yanayoandaliwa na Taasisi ya Istiqaama yenye Makao Makuu yake jijini Dar es Salaam.

Alisema watanzania wengi wamekuwa na tatizo la kulalamika jambo ambalo amelikemea na kuweka wazi kuwa halina afya kwa mustakabali wa vijana.



Kwa upande wake, Waziri wa nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), Mhe. Dkt. Selamani Jafo amewaasa wazazi na wadau mbalimbali kuhakikisha vijana walioweza kuhifadhi kitabu cha mwenyezi Mungu wayaishi maisha yanayo akisi kitabu Allah.

Alisema Wazazi wana kazi kubwa ya kufanya, wameweza kuwasimamia katika hatua za awali hadi kufikia mafanikio ya kuhifdhi kitabu kitukufu, basi waendelee na kazi hiyo ili kuwafanya watoto hao wasibadilike mienendo.

Alisema wazazi wakifanikiwa hapo watakuwa wamefaulu kwani wataacha mtoto mwema ambaye atakuja kumuombea dua mara tu watakapo ondoka katika mgongo wa ardhi.

Akizungumza katika hadhara ya mashindano ya quran yaliyoandaliwa na Taasisi ya Istiqaama Muslim Community Tanzania na kufanyika katika ukumbi wa NSSF uliopo Ilala Jijini Dar es Salaam, Jafo alisema malezi kwa vijana hawa yanapaswa kuendelea.

Vilevile Waziri Jafo amewapongeza Taasisi ya Istiqaama kwa kuendelea kuandaa mashindano hayo, akisema yamekuwa na tija kwa maendeleo ya taifa la Tanzania

“Vijana walioweza kuhifadhi kitabu cha mwenyezi Mungu wanaweza mambo mengi, vijana hawa wakipewa dhamana watakuwa na hofu ya mwenyezi Mungu,” alisema

Pia alieleza kufurahishwa kwake kwa kitendo cha mashindano hayo kuhusisha na upande wa pili wa muungano, kwani anaamini hilo ni jambo zuri lenye kustawisha muungano.

Aidha Jafo hakusita kuonyesha furaha yake kwa kukithiri kwa mashindano ya quran katika miaka ya hivi karibuni na kusema mashindano hayo yanachangia kustawisha Amani.

“Nimefurahi kuona mwendelezo wa mashindano ya quran, April 9, yamefanyika haya ya Istiqaama, April 10, yapo ya Bi Aisha Sururu, April 16, yapo yale ya Asb hab QAF pale viwanja vya sabasaba, April 17, yapo yale ya bara la Afrika yatakayofanyika uwanja wa taifa na kuandaliwa na Al-hkma Foundation, April 24 tunamaliza na mashindano makubwa ya dunia yanayoandaliwa na jumuya ya kuhifadhisha quran chini ya Sheikh Kaporo, matukio yamepanga yakapangika ni rah asana kwa wapenzi wa quran,” alisema.

 Pia Jafo amewatia moyo wanachama wa Taasisi ya Istiqaama Muslim Community Tanzania kwa michango yao wanayotoa kuboresha chama kwani kazi wanayofanya ni uwekezaji mkubwa kwa mwenyezi Mungu.

“Kinachofanyika katika kusomesha vijana kusoma quran na kuhifadhi huu ni uwekezaji wa hali ya juu sana, inawezekana watu wasifahamu hilo, lakini ni wazi kuwa tunawekeza mbele za Allah,” alisema

 Akizungumzaia juu ya serikali kuunga mkono juhudi zinazofanyawa na Taasisi zinazoandaa mashindano ya quran, Waziri Jafo alisema Serrikali ya awamu ya sita inayoongozwa na mama Samia Suluhu Hassani inaunga mkono Taasisi zote za dini, kwani inajua wazi kuwa Amani haiwezi kupatikana bila kuwa na vijana wenye maadili mema.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Jumuiya hiyo, Seif Ali alipongeza wanachama wa Taasisi ya Istiqaama Muslim Community Tanzania kwa michango yao wanayoitoa na kuwaomba kuendelea kutoa kwani uhai wa chama ni michago

“Mwaka jana tulizindua mfumo wa kuchangia chama, kwa sababu ya corona mambo hayakwenda vizuri, lakini wapo waliochangia, mpaka tunafunga mwaka tumepata Mil. 35, tunaamini michango hii itaongezeka tukizingatia kuwa sasa hali imetulia,” alisema

Aidha alisema, Taasisi ya Istiqaama Muslim Community Tanzania inafikilia kujenga Mahadi huko Kigamboni, Jijini Dar es salaam, wanawaomba wanachama kuongeza kasi ya michango.

 

 

 

“Jumuiya yetu inamatawi 25 hapa nchini, tukiangalia hamasa ya usomaji qurani kwa kweli imeongezeka, nguvu inayotumika imeanza kuleta matunda kwa vijana wengi kupenda kusoma qurani,” alisema

Kwa upande wake mshindi wa jumla wa mashindano hayo amewaomba vijana kufanya juhudi ya kukisoma kitabu cha Allah akisisitiza kuwa hakuna kinachoshindikana kama umefanya maamuzi.

Alisema ushindi wake umetokana na juhudi alizokuwa akifanya kwa kushirikiana na Sheikh wake, huku akisema hakuamini kama siku moja angeweza kuibuka kuwa mshindi wa juzuu 30.

Naye mratibu wa mashindano hayo Bw. Khalifa Seif alisema mashindano yam waka huu yamepata mafanikio makubwa kwani vijana wengi walijitokeza kushiriki.

Aidha Khalifa ameungana na Mgeni Rasmi kwa kutoa wa vijana waliohifadhi quran kuendelezwa na elimu zote mbili, ikiwamo ya sekula na dini.

“Watoto wetu wamejitahidi sana katika mashindano haya, wito wangu watoto hawa waendelezwe ili kuweza kupata watoto bora Zaidi, yeyote aliyebeba quran atakuwa bora katika kazi zake lakini hata katika taifa lake,” alisema

“Mimi ndio Kiongozi Mkuu wa kamati ya daawa, kamati ya quraan, ujenzi wa Mahad ni jambo muhimu sana kwa mustakabali wa Jumuiya na waislam kwa ujumla

Hiyo ni kwa sababu kila kitu kinahitaji elimu, na mahadi ni nyumba ya elimu, ishaalah Mahd hii iko njiani kujengwa ni mahadi kubwa ambayo itachukua wanafunzi kuanzia kazi ya msingi ya iptidaiya, thanawi mpaka jamiya,” alisisitiza.

Amewaomba waislam kushiriki katika kheri hizi ili kufanikisha ujenzi wa Mahdi hiyo ambayo ni habari njema kwa waislam. Eneo inapotarajiwa kujengwa kwa Mahdi hiyo ni Mwasonge karibu na Dar es Salaam Zoo, kuna kiwanja cha Istiqaama kisichopungua heka 50, chuo kitajengwa hapo.


 


No comments