Wanafunzi NIT wahusiwa kujiajiri
Mkurugenzi Mkuu wa
Shirika la Viwanda Vidogo (SIDO) Eng. Prof.
Sillvester Mpanduji amewashauri wahitimu wa chuo cha Taifa cha usafirishaji (NIT)
kuangalia fursa mbalimbali za kujiajiri na kwamba Sido ipo tayari kuwasaidia
kitaalamu hasa pale wanapokabiliwa na changamoto za kiutendaji
Akizungumza
katika hafla ya convocation inayotumika kutoa zawadi kwa wanafunzi waliofanya
vizuri chuoni hapo alisema wanafunzi wasifikilie kuajiliwa tu badala yake
wajikite kuangalia jinsi wanavyoweza kujiajiri kupitia utaalamu walioupata
chuoni hapo.
“Nachukua
fursa hii kuwapongeza vijana wote ambao wameweza kumaliza elimu yao, wamejituma
vya kutosha na ndio maana wamehitimu masomo yao, kikubwa wanaenda duniani huko
watakutana na changamoto zingine, ninachokisema ni kwamba wamepata masomo
mazuri kwa hiyo wasitegemee kuajiliwa, wafikilie kujiajili
Wasifikilie
kufanya kazi Tanzania pekee yake, kuna nafasi nyingi hasa ukanda huu wa Afrika
mashariki, kwa hiyo wajikite Zaidi kutafuta fursa huko,” alisema
Sido
inasaidia vijana, kwa hiyo hawa wanafunzi wanaweza kuwa sehehmu ya kuanzisha
viwanda, tumeona hapa kuna mfano wa ndege nzurui tu imebuniwa, kwa hiyo
tunahitaji vijana kama hawa kuwakuza ubunifu wao, wafungue viwanda
kidogokidogo.
Sido
tunatoa mafunzo ya ujasiliamali, mikopo kwa wafanyabiashara hasa wanaotaka
kufungua viwanda lakini pia tunawaunganisha na wadau, kwa hiyo ujio wao katika
shirika hili watapata ufumbuzi wa mambo mengi.
Kwa
upande wake mkuu wa chuo cha Taifa cha Usafirishaji, Prof Zacharia Mganilwa
alisema chuo kimejipanga kuhakikisha kuwa idadi ya wataalamu wa anga kuendelea
kuongozeka.
Alisema
licha ya kwamba mafunzo hayo yana bei kubwa lakini wamejipanga kuona kadri
mwaka unavyozidi kusonga mbele na idadi ya wanafunzi inaongezeka.
“Ni
kweli tasinia ya anga tunao wahimu wachache, sababu kubwa ni haya mafunzo ni
ghali, lakini niwahakikishie watanzania kuwa tunakuwa na wataalamu wa kutosha
kuisaidia taifa.





No comments
Post a Comment