Zinazobamba

Mkuranga wapata uongozi mpya wa soka

 



Na Kahema Juma Fimbo, Mkuranga

Hatimaye chama cha soka Wilaya ya Mkuranga (MDFA) kimefanikiwa kupata safu mpya ya uongozi wa soka ambao wanategemewa kuhudumu kwa kipindi cha miaka minne toka Disemba, 2020 hadi Disemba 2024.

Akizungumza mara baada ya kukamilika kwa uchaguzi, Mwenyekiti mpya wa chama cha soka Wilayani humo, Mwl Minael Njovu alisema uchaguzi ulikuwa na ushindani mkubwa lakini ametoa shukrani kwa kufanyika kwa amani na washindi kupatikana.

Uchaguzi huo ambao mara kadhaa uliahirishwa kutokana na sababu mbalimbali ulishuhudia viongozi mbalimbali wakishinda nafasi zao walizoomba.

Nafasi ambazo ziligombewa katika uchaguzi huo ni pamoja na Mwenyekiti, Makamu Mwenyekiti, Katibu Mkuu, mjumbe wa mkutano mkuu COREFA na mwakilishi wa vilabu.

 Nafasi ya mweka hazina haikugombewa kutokana na kukosa mgombea wa kugombea nafasi hiyo. Mkutano huo ulianza majira ya saa 4 asubuhi na uliiisha kwenye majira ya saa 7 mchana. Uchaguzi ulisimamiwa na katibu wa kamati ya uchaguzi wa chama cha soka mkoa wa pwani(COREFA) Ndugu Masau Bwire.

Wajumbe ambao waliruhusiwa kupiga kura katika mkutano huo walikuwa viongozi wa vilabu vya soka katika wilaya ya mkuranga na viongozi wa chama cha marefa wilayani mkuranga.wagombea wa nafasi hizo mbalimbali walipata nafasi ya kujinadi na kutoa sera zao mbele ya wajumbe hao na wajumbe hao wakasikiliza na kisha kupewa nafasi ya kuwauliza maswali wagombea hao. Wajumbe hao walipiga kura na hatimaye kura zilihesabiwa katika majira ya saa 6 mchana. Baada ya kura kuhesabiwa matokeo yalitangazwa na aliyekuwa katibu wa kamati ya uchaguzi Ndugu Paul Nduru.

Wagombea ambao walishinda katika uchaguzi huo ilikuwa Mwenyekiti alishinda mwalimu Minael Njovu, makamu mwenyekiti Ndugu Kahema Fimbo, nafasi ya katibu mkuu alishinda ndugu Bogras Bryson, nafasi ya mjumbe wa mkutano mkuu wa COREFA alishinda ndugu mwalimu Denis Kalinga na nafasi ya mwakilishi wa vilabu alishinda mwalimu Rajabu Tupa. Baada ya kutangazwa matokeo hayo mwenyekiti mpya alipewa nafasi ya kuongea na kutoa neno la shukrani kwa niaba ya uongozi mpya wa MDFA.

 


No comments