SAMATTA jinsi alivyokuwa nembo ya mpira wa Tanzania
Kahema J Fimbo
Ukizungumzia
nembo ya mpira wa Tanzania kwa sasa kwa kiwango kikubwa utamzungumzia mtoto wa
mbagala kimbangulile Mbwana Ally Samatta.
Samatta
amejitahidi kuitangaza Tanzania katika soka la kimataifa na pia amejitahidi
kujijengea jina na heshima katika maeneo yote hayo ambayo amepita.
Alianzia soka lake katika viunga vya mbagala
na kisha akahamia simba ambako hakukaa sana akahamia kwa matajiri wa soka la Congo
yaani TP Mazembe.
Huko
congo alijijengea heshima na ufalme wake ambako alikuwa hakauki kuzifumania
nyavu na hali iliyompelekea mpaka kupewa tuzo ya mchezaji bora wa afrika katika
wale wanaocheza ligi za ndani ya afrika.
Katika
siku ya tuzo, alipewa tuzo hiyo sambamba na Pierre Emmerick Aubemayang ambaye naye
alipewa tuzo jumla ya mchezaji bora wa afrika.
Katika
kila eneo ambalo amepita Mbwana amekuwa ni mtu ambaye anaacha alama.
Jitihada
zake katika mchezo wa soka zilimfanya aingie katika rada za wababe wa ubelgiji,
timu ya KRC GENK ambao walimsajili na kumhamishia makazi yake huko kwa
wabelgiji.
Ndani
ya nchi ya ubelgiji nako aliendeleza ufalme wake na kufunga magoli mengi na
kujiweka katika kitabu cha magwiji waliowahi kupita katika klabu hiyo.
Hapo
Ubelgiji kulimfungulia njia ya kuweza kushiriki katika ligi ya Europa ambako
alizifunga na kuingiza jina lake na kuwa ni mtanzania wa kwanza kufunga goli
katika shindano hilo na hakukaa sana timu yake ikabeba ubingwa wa ligi ya
Ubelgiji na kisha kumpatia nafasi ya yeye kushiriki katika ligi ya klabu bingwa
ulaya.
Katika
ligi ya klabu bingwa ulaya alipangwa kundi moja na timu kubwa za ulaya kama
vile Liverpool na Napoli na kujikuta akicheza mechi moja na mastaa wakubwa
barani ulaya na huku akikabwa na mabeki bora kwa sasa katika viwango vya dunia
yaani nawazungumzia Virgil Van Dijk pamoja na Wengineo.
Katika
klabu ya mabingwa alizidi kupandisha thamani yake kwa kumfunga kipa bora
Alisson Becker wa Liverpool.
Ufundi
wake wa kupachika mabao uliwafanya mabosi wa Aston Villa kumsajili katika timu
yao na kisha kumhamishia nchi ya uingereza. Alipofika Uingereza amecheza kidogo
na hakuweza kuwika sana na wakongwe hao wa uingereza wakamhamishia katika nchi
ya uturuki katika klabu ya Fenerbache kwa mkopo ambapo anacheza huko.
Kuna
faida nyingi sana kwa watanzania kwa Samatta kununuliwa nchini Uturuki. Mosi
kwa kucheza huko kutamsaidia kutengeneza fursa kwa wachezaji wa kitanzania
kusajiliwa huko.
Kwa kitendo cha yeye kusajiliwa huko
ametambulisha vilabu ya uturuki kwamba nchi ya Tanzania ina vipaji vya soka na
kwa sasa maskauti wa vipaji wa timu za soka huko uturuki watakuwa wameweka rada
zao kwa vijana wa kitanzania ambao watakuwa wanaibukia.
Pili
amefungua fursa za utalii kwa nchi ya Tanzania kwani kuna waturuki ambao
wataijua nchi ya Tanzania kupitia yeye na watakuwa wana shauku ya kuja
kutembelea Tanzania kuja kujionea vivutio vya utalii.
Kwa
fursa hizo nina rai kwa shirikisho la mpira lishirikiane vizuri na bodi ya
utalii kualika vilabu vya nchi ya uturuki kuja kucheza mechi zao za kujiandaa
na msimu(pre-season) huku Tanzania na kisha baada ya kucheza mechi hizo wapate
fursa ya kwenda kuandalia vivutio vya utalii.

No comments
Post a Comment