Zinazobamba

Ligi ya watoto yaja...Shule zashauriwa kuchukua fomu

 





Shirikisho la shule za michezo Tanzania(TASCA) lina mpango wa kuasisi ligi za watoto ambazo zitachezwa kwa ngazi mbalimbali kuanzia ngazi za wilaya kisha mkoa na kisha kanda.

Ligi hizo zitakuwa za makundi mbalimbali kuanzia kundi la chini ya miaka 15, chini ya miaka 18, na kisha chini ya miaka 21. Ligi hizo zitaratibiwa na TASCA kwa kupitia wawakilishi wake katika kanda tofauti.

 Hayo yamesemwa kupitia ujumbe ambao ulisambazwa kwa vyombo vya habari vya mitandaoni

Shirikisho hilo ambalo linatimiza mwaka mmoja toka lisajiliwe limezitaka Shule ambazo zina mpango wa kushiriki katika ligi hiyo ziwasiliane na wawakilishi wa kanda wa TASCA au ziwasiliane na kamati kuu kwa ajili ya kupewa formu ya ushiriki na gharama ya formu hizo ni kiasi cha shilingi za kitanzania elfu hamsini.

Wawakilishi wa TASCA wanatakiwa wawe makini kuhakikisha kwamba shule zitazoshiriki katika kanda husika zinaleta wachezaji ambao watakuwa wana umri husika.

wachezaji ambao watakaowakilisha timu katika mashindano hayo watatakiwa kuwasilisha nakala za vivuli(photopy) za vyeti vyao vya kuzaliwa. Vyeti hivyo vitawasilishwa kwa waratibu wa mikoa na kisha vitawasilishwa kwa kamati kuu ya taifa ya TASCA kwa ajili ya kuweka kumbukumbu na kuzihakikisha kama ni za kweli.


No comments