Zinazobamba

TRA YAZIDI VUNJA REKODI YA MAKUSANYA YA MAPATO,YATOA TAARIFA YAKE KWA KIPINDI CHA MIEZI SITA,SOMA HAPO KUJUA

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEi2ZP1AvY3HGOGIF4DeD-KR4OOrHN3QJ1L3Q1V0pUNppzF8WzSE_AVKqbib-TpIBh7ugwPaSSLv7hHuQWbwNGkkK78ljbYTmJUuS4zma47_Je611QCGDqROmK2AXZHcyZWgTOV6Rm1eeLI/s640/kayombo1.jpg
NA KAROLI VINSENT
MAMLAKA ya Mapato nchini (TRA) imetangaza kuvunja rekodi ya ukosanyaji mapato katika mwaka wa fedha 2016-2017 katika kipindi cha miezi sita toka Julai 2016 hadi Desemba  2016  mwaka jana baada kukusanya kodi ya jumla ya shilingi trioni 7.27 ambapo ni sawa na asilimia 12.74 ya ongezeko la mapato ikilinganishwa na Trion 6.44 ambazo zilikusanywa kipindi kama hicho mwaka wa fedha 2015/2016.
Akizungumza na Waandishi wa  habari leo Jijini Dar es Salaam,Mkurugenzi wa Huduma na Elimu ya Mlipa kodi wa TRA,Richard Kayombo amesema ongezeko hilo la mapato limetokana  na Mamlaka hiyo kuziba mianya ya ukwepaji kodi jambo lilochangia mapato hayo kuongezeka.
“Ongezeko hili limetokana  na jitihada mbali mbali zilizofanywa na TRA katika kuongeza ufanisi wa ukusanyaji kodi,kuhimiza maadili mema kwa watumishi,kuboresha mifumo ya ukusanyaji kodi,kushirikiana na vyombo vya vingine vya dola na wananchi kuziba mianya upotevu wa mapato’amesema Kayombo.

Kayombo akichanganua mlinganisho wa ukusanyaji wa mapato kwa mwaka wa fedha 2015-2016 na 2016/2017 amesema Julai 2015-2016  Mamlaka hiyo ilikusanya Bilioni 925.384.7 ambapo katika kipindi cha mwezi kama huo katika Mwaka 2016-2017 walifanikiwa kukusanya Trioni 1.068.458.6 sawa ongezeko la asilimia 15.57.
Pia katika mwezi Agosti mwaka wa fedha 2015-2016 walikusanya Bilioni 923.316.9  ambapo pia katika kipindi kama cha mwezi huo katika mwaka wa fedha 2016-2017 wamefanikiwa kukusanya Trioni 1.154.222.5 ambapo ni sawa na asilimia 25.01.
Kayombo amesema Semptemba katika mwaka wa fedha 2015-2016 walikusanya trion 1.132.310.3 ambapo katika mwezi wa kama huo kwenye mwaka wa fedha 2016-2017 wamefanikuwa kukusanya Trion1,378.048.9 ambapo sawa na ongezeko la asilimia 21.70.
Octoba katika mwaka 2015-2016 walikusanya trion 1.037.179.8 na pia katika mwezi kama huo  mwaka 2016-2017 walikusanya trion 1.131.094.9 ambapo sawa na ongezeko la  asilimia 9.05.
Kayombo ameongeza kusema kuwa katika mwezi Novemba mwaka 2015-2016 walikusanya  trioni 1.027,393,6 na kipindi kama hicho katika mwaka wa fedha 2016.2017 wamefaikiwa kukusanya trioni 1,123,509.7 sawa na ongezeko la asilimia 9.30.
Hata hivyo pia katika mwezi Disemba katikamwaka 2015-2016 walikusanya Trion 1,403,189.8 huku pia katika kipindi kama hicho katika mwaka 2016-2017 walifanikiwa kukusanya trion 1,414,921.8 sawa na asilimia 0.84.
Pamoja na hayo Kayombo  amewataka wafanyabiashara wote  kulipa kodi stahiki kwa hiari na wakati ili serikali ipate Mapato yake kwa wakati ambayo amedai yataweza kuwahudumia Wananchi wake kikamilifu.
Pia amewahimzia  wafanyabiashara wote wenye madeni ya Nyumb a kujitokeza kuonana na Mameneja wa Mikoa na Wilaya kujadiliana jinsi watakavyolipa madeni yao bila kuathiri biashara zao.