UKAWA WAANZA KUMSULUBU LIPUMBA NA GENGE LAKE,WAIBUKA NA KUTOA MSIMAMO MZITO,SOMA HAPO KUJUA
Umoja wa Katiba ya Wananchi
umedhamiria kwenda mahakamani kumshtaki Prof. Lipumba na Msajili wa Vyama vya
Siasa nchini kutokana na mgogoro unaoendelea ndani ya Chama cha Wananchi (CUF).
Katika kikao walichofanya jana, UKAWA walipitisha maazimio kukabiliana na mgogoro unaoendelea ndani ya CUF. Maazimio hayo ni pamoja na;-
Hatumtambui Prof. Lipumba kama mwanachama wa
CUF na Mwenyekiti mwenza wa UKAWA
UKAWA wanautambua uongozi wa Julius Mtatiro na
Maalim Seif
Wanachama wa vyama vinavyounda UKAWA wasitoe
ushirikiano kwa Prof. Lipumba na washirika wake
Wenyeviti wa mitaa, vijiji, Madiwani, Wabunge
wasitoe ushirikiano kwa Prof. Lipumba na washirika wake
Wabunge wote wanaomuunga mkono Prof.
Lipumba watatimuliwa ndani ya Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni
Ushirikiano wa kisiasa Tanganyika na Zanzibar
utashughulikiwa na UKAWA
Mawakili wa UKAWA watamfunguliwa mashtaka
Msajili wa Vyama vya Siasa nchini kwa matumizi mabaya ya madaraka na
Mawakili wa UKAWA watamfungulia mashtaka Prof.
Lipumba.
Kwa upande wake Prof. Lipumba aliwataka wanachama wa
CUF kuwa wamoja na kusema kuwa yeye hajali kuhusu UKAWA kikubwa anachoangala ni
kuijenga upya CUF.