Zinazobamba

TRL YAZINDUA HUDUMA MPYA YA USAFIRI WA TRENI,SOMA HAPO KUJUA



TRL NE

 

Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania chini ya Rais wake John Pombe Magufuli, imeendelea kufanya jitihada ili kuimarisha suala la usafiri kwa wananchi  wake ambapo imeshuhudiwa uwepo wa Magari ya Mwendo Kasi, Usafiri wa Treni kwa safari za Stesheni Pugu, Stesheni Mwakanga, halikadhalika uwepo wa Treni ya Kasi maarufu kama Deluxe, lakini Serikali kupitia Kampuni ya Reli Tanzania imeamua kuja na Mwarobaini mwingine wenye tija kwa wananchi.


Ambapo siku ya leo jijini Dar es Salaam Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa TRL Focus Makoye Sahani ameeleza kuwa uongozi wa Kampuni ya Reli Tanzania imeamua kuongeza safari ya tatu ya treni ya abiria ya kawaida kwenda bara, ambayo itaanza rasmi safari zake Jijini Dar es Salaam siku ya Jumapili, Septemba 4, 2016 majira ya Saa tisa, huku akifafanua kuwa treni hiyo ya huduma ya kawaida itakuwa na mabehewa 12 kutoka Dar es Salaam ikiwa na mabehewa 8 ya daraja la 3, mawili ya daraja la pili yatakayo muwezeha abiria kupata sehemu ya kulala, na mawili daraja la kwanza na katika stesheni za Morogoro na Dodoma yataongezwa mabehewa mawili ya daraja la tatu.


Aidha ameeleza kuwa Treni ya Deluxe imebadilishwa siku ya kuondoka badala ya Jumapili ambapo kwa sasa kuanzia Septemba Mosi, 2016 itakuwa inaondoka siku ya Alhamis saa 2 asubuhi kutokea kituo kikuu cha Dar es Salaam, halikadhalika mabadiliko hayo yataongeza safari za treni ya kwenda Mpanda kwa kutokea Tabora badala ya safari mbili kwa sasa zitakuwa tatu kwa wiki ambazo ni Jumatatu, Jumatano na Jumamosi.
Pia Kaimu huyo Mkurugenzi Mtendaji wa TRL amesema kampuni hiyo ya TRL imefanya uamuzi wa kihistoria wa kupeleka huduma za kuuzwa tiketi za safari za Mjini Kasulu zitakazo anza Septemba Mosi, hivyo itafungua kituo cha Reli ambacho kitafanya kazi ya kutoa huduma hiyo kwa wasafiri wanaotoka Kasulu na Maeneo ya jirani, 
Hivyo Kaimu huyo Mkurugenzi Mtendaji amewataka wasafiri na wananchi kwa ujumla nchini, hususani kwa wale wa Mpanda na Kibondo kutumia fursa ya kuongezwa safari na huduma kuletewa karibu kwa kufuata sheria, taratibu na kanuni ili hatua iliyochukuliwa na TRL iwe na tija ilyokusudiwa