RC MAKONDA AIBUKA NA HIKI LEO,SASA AJITOSA KUWAJENGEA JENGO BAKWATA,SOMA HAPO KUJUA
|
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda pamoja
na Sheikh Mkuu wa Tanzania,Mufti,Abubakary Zubeir wakitazama mchoro wa
ramani wenye ghorofa tatu,ambapo ujenzi wake utagharimu zaidi ya shilingi
bilioni tano,ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya ujenzi wa jengo jipya la Baraza
hilo.
,kulia ni Sheikh Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam , Alhaji Mussa Salum . |
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda
amekabidhi mchoro wa ramani wenye ghorofa tatu kwa uongozi wa Baraza Kuu la
Waislamu nchini,BAKWATA ikiwa ni maandalizi ya ujenzi wa jengo jipya la Baraza
hilo.
Pamoja na kukabidhi ramani hiyo, Mkuu wa Mkoa huyo
amesema jengo hilo litagharimu kiasi cha fedha 5, 080, 155, 600 ili kukamilika.
Pia amesema jengo hilo mpaka kukamilika litakuwa la
kipee na kupewa hadhi kama Taasisi kubwa
ya Kiislamu na kusisitiza ujenzi wa jengo hilo hautazidi miezi 14.
Amesema amekabidhi mchoro huo kutokana na kutambua na
kuthamini umuhimu wa BAKWATA katika Taifa pamoja na kuwataka Waislamu na wasiokuwa waislamu kujitokeza katika kutoa misaada hiyo.
Pia ametoa shukrani kwa waislamu wa mkoa wa Dar es
Salaam kwa kushereheka nao pamoja katika
Mfungo wa Mwezi Mtukufu wa Ramadhani, ambapo amesema mwezi
huo ndio uliokuwa chimbumbo la ujenzi wa jengo hilo la BAKWATA.
Akitoa shukrani zake kwa Mkuu wa Mkoa huyo, Sheikh Mkuu wa Tanzania, Mufti Abuubakari Zuberi amewataka Waislamu kumuunga mkono Mkuu wa Mkoa huyo ikiwa kuwataka kuamini ya kuwa na haki ya kupokea misaada kama Waislamu.
huo ndio uliokuwa chimbumbo la ujenzi wa jengo hilo la BAKWATA.
Akitoa shukrani zake kwa Mkuu wa Mkoa huyo, Sheikh Mkuu wa Tanzania, Mufti Abuubakari Zuberi amewataka Waislamu kumuunga mkono Mkuu wa Mkoa huyo ikiwa kuwataka kuamini ya kuwa na haki ya kupokea misaada kama Waislamu.