MBUNGE KUBENEA AANZA KULITIKISA BARAZA LA MAWAZIRI JPM,WAZIRI WAKE AIBUKA NA KULIA NA GAZETI LAKE,SOMA HAPO KUJUA

NA KAROLI VINSENT
MBUNGE wa Ubungo,Saed Kubenea ambaye ni Mmiliki wa
Kampuni ya Hali halisi Puplish ambao ni wachapishaji wa Gazeti la Mwanahalisi
na Mseto teyari kwa sasa ameanza
kulitikisa baraza la Mawaziri la Rais John Magufuli ndivyo naweza kusema baada Mmoja wa mawaziri wa
Magufuli kuibuka na kutaka alipwe bilioni 1 na kampuni hiyo kwa madai kuwa
amechafuliwa.
Anayetaka malipo hayo ni Naibu Waziri wa Ujenzi,
Uchukuzi na Mawaliano,Mhandisi Edwin Ngonyani amedai kuwa atamfikisha Mahakamani
Mmiliki wa Gazeti la Mseto ambaye ni Kubenea,Mwandishi wa Gazeti hilo,Josephat
Isango pamoja na Mchapajishaji wa Gazeti hilo kutokana na kuandika habari
anayodai imechafua.
Mhandisi Ngonyani ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la
Natumbu ameyasema hayo leo Jijini Dar es Salaam wakati wa mkutano na waandishi
wa habari, amesema Gazeti la Mseto la Alhamisi ya tarehe 4 mwezi huu Gazeti
hilo lilibeba kichwa cha habari “Waziri wa amchafua JPM”
Amedai habari hiyo iliyochapishwa ukrasa wa mbele
huku ikiweka picha yake pamoja na picha ya Rais John Magufuli huku taarifa hiyo
ikimtaja Mhandisi Ngonyani kuwa wakati alipokuwa mkurugenzi wa Stamico alipokea
fedha toka wafanyabiasha zilizodaiwa
kumsaidia mpaka kuwa mbunge na baadaye kufanikiwa kuwa Naibu Waziri.
Amejitetea kuwa Habari hiyo ni ya uongo yenye lengo
la kumchafua yeye kwa jamii pamoja kuweka nia hovyo kwa Rais Magufuli kuwa
alisaidiwa na wafanyabiasha mpaka kupata madaraka ambapo Rais Magufuli kila
mara amekuwa akipinga kuwa yeye hakusaidiwa na mfanyabiashara.
Mhandisi huyo ameenda mbali na kudai kuwa hata (Document)
iliyochapishwa ukrasa wa mbele ambayo mwandishi wa habari hiyo,Isango ameitumia
kama chanzo cha habari ni ya kufoji kwani hata tarehe iliyoandikwa wakati yeye
akisaini barua hiyo alikuwa teyari ameacha kazi.
Amesema baada ya kusoma habari hiyo na kujilizisha
siyo ya ukweli ameliandikia baraua gazeti hilo ndani ya siku saba kumuomba
radhi kwa uzito ule ule habari ilivyoandikwa na kutoa fidia bilioni 1 kwa kile
anachodai kuchafuliwa hadhi yake,
Amesema endapo Gazeti hilo likikataa kufanya
hivyo,basi atamfikisha mmiliki wa Gazeti hilo,Mwandishi wa Habari hiyo,Josephat
Isango pamoja na mchapishaji wake mahakamani ili hatua zaidi zichukuliwa.
WADAU
WANENA.
Wakizungumzia hali wadau mbali mbali wa masuala ya
habari wamesema hatua ya Mhandisi Ngonyani inaweza ikawa ya kutisha kwa
sababu kuwa viongozi wengi
hawaitekelezi.
“Ujue Yule mwandishi Isango hawezi akaandika habari
ile kwa kutunga,ni jambo la kutafakali tu hivi tangu viongozi hawa
waandikwe kwenye magazeti ni mara ngapi
wanakuja na matamko na vitisho kama hivi na wanaishia kuwa kimya, “amehoji
mwandishi mmoja wa Gazeti linalotoka kwa siku.