MAJANGA TENA CLOUDS TV NA REDIO, ITV,TCRA YAVIPIGA PINI,MSIGWA AIPONZA ITV,SOMA HAPO KUJUA

MAMLAKA ya Mawasiliano nchini (TCRA)imevipiga faini
ya milioni 5 vituo vya utangazaji vya
Clouds Redio na kituo cha Independent
Television (ITV ) huku pia ikipiga faini ya milioni 4 kituo cha Clouds Tv pamoja kuvipa onyo kali vituo hivyo,baada ya kukiuka kanuni za utangazaji .Anaandika
KAROLI VINSENT endelea nayo.
Akitoa hukumu hiyo leo Jijini Dar es
Salaam,Mwenyekiti wa Kamati ya Maudhui wa (TCRA)Mapunda amesema vituo vyote vimekiuka kanuni ya utangazaji ya mwaka
2005 baada ya kutenda makosa tofauti ambayo yenye lengo la kuipotosha jamii.
Mapunda amedai kuwa mnamo tarehe 9/05/2016 kituo cha
Clouds Redio katika kipindi cha
Jahazi kilikiuka kanuni hizo baada ya mtangazaji wa kipindi hicho Eprahimu
Kibonde kushabikia kijana mwenye umri wa miaka 14 ambaye alifanya
mapenzi ya mbuzi.
Amesema katika kipindi hicho mtangazaji huyo alionekana
kushabikia hali hiyo baada ya kusema Kijana aliyefanya mapenzi na mbuzi ilitakiwa
atoe posa kwa mbuzi huyo, jambo ambalo linakwenda kinyume na sheria ya
utangazaji ya mwaka 2005
Na.5(c),5(g),14(1).
Amesema baada ya kamati yake kubaini makosa hayo
waliwasilina na uongozi wa Clouds media kutaka kupata utetezi wa kosa hilo
lakini mmiliki wa Clouds redio Ruge Mtahaba ambapo katika maelezo yake ya awali
alikili kosa kwa watangazaji hao kutozingatia sheria hiyo huku akiomba Mamlaka
hiyo kuwasamehe.
Mbali na kipindi hicho pia Kamati hiyo imebaini
ukiukwaji wa sheria hiyo kwenye kipindi cha Power Breakfast kinachorushwa kila
siku saa 12 asubuhi hadi saa 10 asubuhi ,amedai kuwa siku ya tarehe 18/5/2016 katika redio hiyo watangazaji wa kipindi hicho walitumia maneno
yasiyo na staha.
Amedai kuwa katika kipindi hicho watangazaji hao walisoma
taarifa kwenye magazeti inayosema “Mtoto wa miaka mitatu apandikishwa Uume”
huku watangazaji hao wakiwasilisha taarifa hiyo kwa mzaha yenye kujaa kushabikia
masuala ya ngono na kushindwa kusimamia kanuni za utangazaji.
Hata hivyo,amesema katika kipindi hicho kilikuwa
hakina mtaalamu wa masula ya kitabibu wenye kutoa ukweli juu ya taarifa hiyo
kutoka kwenye magazeti.
Mapunda amesema baada ya Mamlaka hiyo kubaini
ukiukwaji huo wa kanuni waliwasiliana na Uongozi wa Redio hiyo ambapo utetezi
wake walisema watangazaji hao
hawakufanya makosa kwani walitoa taarifa ilivyo kutoka kwenye magazeti.
Hata hivyo,Mapunda amesema utetezi wa Clouds Redio haukuwa
na mshiko kwani watangazaji hao walishindwa kusimamia sheria ya utangazaji ya
2005 inayokataza kurusha maudhui yenye matusi kuanzia saa 11.30 alfajili hadi saa 3 usiku kwani mda
huo watoto wanakuwa macho.
MAKOSA YA
CLOUDS TV NA ITV.
Mapunda amesema mnamo tarehe 15/06/2016 kituo cha
Independent television cha Dar es salaam(ITV) katika kipindi cha Kumekucha
kilichorushwa hewani kati ya saa 1.00 asubuhi
na saa 1.30 asubuhi kilitangaza uchambuzi wa Bajeti ya serikali ya mwaka 2016/2017 ambapo
mtangazaji wa kipindi hicho,Godfrey Monyo
alifanya mahojiano na Mbunge wa Iringa Mjini,Peter Msigwa.
Amesema katika kipindi hicho Msigwa alitamka kwamba Naibu Spika Dkt Tulia Akson
kuwa anavaa “Pumpers” kwa ajili ya kujisaidia kwa sababu amekuwa hawaachii watendaji wengine
kiti na cha spika kwa ajili ya kuliongoza Bunge.
Mapunda amesema katika kipindi hicho mtangazaji
alishindwa kuudhibiti mjadala huo jambo ambalo lilipeleka lugha za matusi
kutoka.
Aidha,Mamlaka hiyo baada ya kubaini makosa hayo
walifanya mawasiliano na Uongozi wa ITV,ambapo Mhariri wa kituo hicho,Steven
Chuwa alitoa utetezi kuwa kipindi hicho kilikuwa live (moja kwa moja) kwahiyo
ni vigumu mtangazaji kuzuia hali hiyo
pamoja na hata hadhi ya Mbunge Msigwa kwenye jamii kwani yeye mwenyewe angejua
aina ya maneno kutamka.
Mapunda amesema baada ya utetezi huo,Mamlaka hiyo
ikabaini kituo hicho kimekuka kanuni ya utangazaji ya mwaka 2005 inayokataza
kituo kutoa maauzi yenye kugombanisha umoja na mshikamano na kutoa maneno yenye
kuudhi Mamlaka za serikali.
Katika hatua
Nyengine TCRA imkipiga faini ya Milioni 4 kituo cha Clouds Television ambao
inadaiwa mnamo tarehe 22/05/2016 katika kipindi cha “Hip Hop” kinachorushwa
hewani saa 8.00 mchana hadi saa 12.00 jioni walirusha video ya “Thank for Coming”
ya mwanamuziki F.A pia katika kipindi
hicho walirusha wimbo wa “Lil Bebbie” unaoitwa Break it Down ambapo katika
nyimbo hizi zilionyesha maudhui ya baadhi ya wanawake wanaovaa nguo za uchi.
Amedai kuwa jambo la kuonyesha video hizo ni kinyume
na sheria ya utangazaji ya mwaka 2005 inayokataza kuonyesha vipindi kama hivyo
kwenye mda ambao watazamaji ni watoto.
Aidha,Mapunda amesema vituo vyote vilivyopewa adhabu
hiyo watakiwa kulipa fedha hizo ndani ya siku 30 huku rufaa zikiwa wazi kwa
kituo ambacho hakijalizika na hukumu hizo.