Zinazobamba

HATIMAYE SASA IDADI YA WABUNGE WA VITI MAALUM YATOKA RASMI,CCM,CHADEMA CUF WAAMBULIA HAWA,SOMA HAPO KUJUA


NA KAROLI VINSENT
TUME ya Taifa uchaguzi nchini,NEC imetangaza  idadi ya wabunge wa viti maalum ambapo vyama vya Chama cha Mapinduzi CCM , chama cha Demokrasia na Maendeleo Chadema pamoja na Chama cha Wananchi CUF vyote kwa pamoja vimepata wabunge baada ya kupata angalau asilimia 5 ya kura halali za wabunge nchi nzima.
       Akizungumza na waandishi wa habari leo Jijini dare s Salaam,Mwenyekiti wa NEC,Jaji Damian Lubuva amesema Chama cha CCM kilipata jumla ya kura milioni 8.3 na kufanikiwa kupata idadi ya wabunge 64 wakati chama cha Chadema kimepata kura milioni 4.7 na kupata wabunge wa vita maalum 36,
     Sanjari na vyama hivyo,Jaji Lubuva pia amekitaja chama kingine kilichopata wabunge wa viti maalum ni chama cha Wananchi CUF kimepata  kura milioni 1.2 na kufanikiwa kupata wabunge wa viti maalum 10.
       Hata hivyo jaji Lubuva ameainisha kuwa idadi ya wabunge wa viti maalum ilitakiwa kuwa ni 113 lakini kwa sasa wamegawa wabunge 110 huku wabunge watatu waliobakia watapatikana baada ya kumalizika kwa majimbo tisa ya ubunge ambayo hayajafanya uchaguzi,

      Pamoja na hayo amebainisha kuwa Majina ya wabunge husika ya Viti maalum yatatolewa na vyma husika baada ya tume kuhakiki majini hayo na teyari wameyarudisha kwenye vyama husika

Hakuna maoni