POLISI WAENDELEA KUISAKAMA CHADEMA NA UKAWA,WAIPIGA TENA MARUFUKU MKUTANO WAKE WA NCHI NZIMA JUMAPILI,SOMA HAPO KUJUA
POL
JESHI la Polisi nchini limepiga marufuku mikutano
yote ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo Chadema iliyotarajiwa kufanyika kesho kutwa Jumapili
nchi nzima.Anaandika KAROLI VINSENT endelea nayo
Akitoa
katazo hilo, leo jijini Dar es Salaam wakati wa mkutano na waandishi wa habari na Msemaji wa Jeshi la Polisi nchini,Advera Bulimba
ambapo amesema Jeshi la Polisi limepata
barua kutoka kwa Chadema iliyokuwa inataka kuomba ruhusa ya kufanyika kwa
mkutano kila mkoa ambao ulitakiwa kufanyika jumapili wenye lengo la kutoa sera
kwa wananchama wake.
Bulimba amesema mara baada ya Jeshi hilo kupata
barua hiyo wakafanya Tasmini na kubaini bado nchini kuhali tata ya usalama.
“Tumekata mikutano hii,baada ya kubaini kuna
mihemuko ya kisiasa ndani ya jamii yetu,hivyo
mikutano au maandamano ya aina hiyo inaweza kusababisha uvunjifu wa
amani endapo ikutuhusiwa”amesema
Bulimba.
Ameongeza kuwa “Jeshi la Polisi bado linasisitiza
katazo lake la awali liliozuia mikutano
na maandamano mpaka hapo hali itakapotengamaa”
Hata hivyo,Jeshi hilo la Polisi nchini linatoa wito
kwa wananchi wote nchini kuendelea kutoa ushirikiano katika kipindi chote cha
uchaguzi kwa kujiepusha na vitendo vyovyote vitavyoleta uvunjifu wa amani
Hakuna maoni
Chapisha Maoni