Zinazobamba

MRADI WA TRANS -SEC KUNUFAISHA WAKULIMA WADOWADOGO,PROF TUMBO TOKA SUA ASEMA HAIJAWAHI KUTOKEA,

Meneja mradi wa Trans -Sec Prof Siza Tumbo akifafanua malengo mazima ya mradi wa Tarsn Sec Huko mkoani Dododma na Morogoro.Tumbo amesema mradi huo ni shirikishi na kwamba unatarajiwa kuleta mageuzi makubwa katika suala zima la upatikanaji wa chakula cha uhakika.
Profesa kutoka Dododma akifafanua jambo katika mkutano huo wa wadau wa kuutambulisha mradi pamoja na changamoto za wakulima ambazo wameziona katika hatua yake ya awali ya kkutekeleza mradi huo huko katika vijiji. Prof amesema wakulima wamesema tatizo lao kubwa ni upatikanaji wa pemabejeo ambazo zinadaiwa kutofika kabisa katika vijiji vya mbali
Ahadiel Mmbughu akifafa nua jambo katika mkutano huo

Chuo cha Sokoine Sua kikishirikiana na Chuo cha Ujerumani , vinatarajiwa kuondoa tatizo la uhaba wa chakula cha uhakika katika maeneo ya walala hoi huko vijijini kufuataia kkuja na mradi mshirikishi uliolenga kuangalia mnyororo mzima wa thamani ya chakula ili kubaini changamoto zake na kuja na majawabu yatakayohakikisha chakula kinapatikana kwa wingi,

Akiutangaza mradi huo kwa wadau mbalimbali wakiwemo wakulima wenyewe, wamiliki wa viwanda, masoko, Mineja mradi toka Chuo cha kilimo Sua Prof. Siza Tumbo amesema mradi huo wa miaka mitano umelenga kuhakikisha uhakika wa chakula unaongezeka kwa asilimia kubwa huko vijijini,
Prof. Tumbo amesema, hali ilivyo sasa ni kwamba hakuna chakula cha uakika huko vijini na kwamba mradi umekuja katika wakati muafaka wa kuondoa changamoto ya kutopatikana kwa chakula cha uhakika,

wadau katika mkutano huo wakifuatailia mada zinazowasilishwa na wataalam,

Mradi huo unaotarajiwa kughalimu jumla ya ERO milion 7, unadaiwa kumkomboa mkulima mdogo kwani ni mradi unaoatarajiwa kuwashirikisha wakulima wengi katika hatua zake za uzalishaji, 
Prof Tumbo amesema mradi huo utashirikisha jumla ya vijiji viwili toka katika mikoa miwili ya Dododma Na Morogoro ambapo katika vijiji hivyo jumla ya wakulima 150 kila kijiji wanatarajiwa kushiriki katika utekelezaji wa mradi huo.
 Katika hatua zake za kwanza, mradi umebaini baadhi ya changamoto zinazopelekea chakula cha uhakika kisipatikane nazo ni pamoja na sewrikali kushindwa kufikisha mbolea kwa wakati, kutoa kodi kubwa ya mazao changamoto ambazo zinawavunja nguvu wakulima kwa kiasi kikubwa
Picha ya pamoja ya wadau hao waliokutana katika mkutano huo wa siku mbili uliofanyika huko ubungo jijini Daresalaam.


No comments