MAJANGA YAZIDI KUIKUMBA CLAUDS RADIO,SASA TCRA YAZIDI KUIKABA KOO RADIO HIYO SOMA HAPA KUJUA
Mwenyekiti wa kamati ya maudhui ya TCRA, Mhandisi Margaret Tabu Munyagi, akifafanua jambo mbele ya Waandishi wa Habari picha na Maktaba
Na Karoli
Vinsent
MAJANGA
yanazidi kuiandama kituo cha Radio cha Clauds Fm,baada ya leo Mamlaka ya
Mawasiliano nchini TCRA,kuipiga Faini ya Milioni Nane za kitanzania kutokana na
kutangaza Kipindi kisichokuwa na maadili kwa watanzania.
Kwa Mujibu wa Taarifa iliyotolewa na
Mamlaka ya Mawasiliano nchini TCRA kwenye vyombo vya habari na
kusainiwa na Mwenyekiti wa Kamati ya Maudhui ya vipindi vya Radio nchini kutoka
kwenye Mamlaka hiyo,Eng Margalet T Munyangi inasema maamuzi hayo yamefikiwa kutokana na kuridhishwa na
ushahidi waliokuwa nao,
Ambapo Mamlaka hiyo inasema Faini hiyo
inatokana na kituo hicho kukiuka sheria ya Utangazaji nchini ya mwaka 2005,kwa
kuruhusu Kipindi cha Njia panda kilichorushwa tarehe 15-06-2014 kwaanzia saa
8.00 mchana hadi saa 10.00 jioni,katika kipindi hicho ilikuwa na mada ya Safari
ya kuzimu,
Mada hiyo ilikuwa ni ya kufikirika na
kichawi zenye kudanganya umma ambao walikuwa wakisiliza kipindi hicho,kwani
kufanya hivyo kituo hicho cha Radio kilikiuka sheria ya utangazaji ya mwaka
2005 namba 5(a) (b) (c) (f) (g) (h) na 14 1 na 15 b ambapo kifungo hicho
kinakataza Radio kutangaza vipindi visivyokuwa na Maadili.
Aidha Mamlaka hiyo Imesema kituo hicho
kimekiuka tena sheria hiyo ya Utangazaji mwaka 2005 kifungu namba 22(1) ,(3) (a),(b)
kwa kushindwa kutoa taarifa kwenye gazeti la kuhusu taarifa ya vipindi vyake
kwa umma,ambapo sheria hiyo inavitaka vituo vyote vya Radio kutoa taarifa ya
vipindi vyake kwenye Mamlaka hiyo pamoja na kwenye Gazeti lakini Clauds
hawakufanya hivyo.
Vilievile Mamlaka hiyo imesema baada
ya kubaini makosa hayo kamati kuu ya maudhui ya Mamlaka ya Mawasiliano Nchini
TCRA ilikaa na kuanza kuchukua ushahidi pamoja na kuwaita Wahusika wa Radio
hiyo kuja kutoa utetezi wao,
Ndipo Mkurugenzi wa Radio hiyo Ruge Mtahaba aliitwa kuja kuto
utetezi lakini naye alikiri kosa kwa
kuruhusu kipindi hicho na kushindwa kufanya usahihi wa Taarifa hiyo baada ya
kugundua kuna makosa,
Kutokana ushahidi huo Mamlaka
hiyo imewapiga faini Radio hiyo ya Milioni Nane za kitanzania na kuitaka Radio
hiyo ilipe pesa hizo ndani ya mwezi Mmoja kutoka siku ya uamuzi ambao ni leo.
Mamlaka hiyo imetoa rai kwa
kituo hicho kutangaza kwa kutumia weredi na maadili kwani wakiendelea hivyo
mamlaka hiyo haita wafumbia macho na kuzidi kusema itachukua hatua kali ikwemo
hata kuwanyang’anya leseni.
Huu ni Mwendelezo wa Majanga
yanayozidi kuiyandama Clauds Radio kutoka na hivi sasa Radio hiyo kuingia
Mgogoro na umoja wa Kutetea Katiba ya Wananchi UKAWA kutokana na Radio hiyo kusema haita soma habari zinazohusu umoja huo kwa Madai umoja
huo ni Wabinafsi.
UKAWA ni muunganiko wa vyama vya
Kisiasa ikiwemo Chadema,CUF,NCCR,mageuzi,NLD pamoja na wajumbe wengine 201
waliochaguliwa na Rais umoja huo umejiapiza kutorejea bungeni kwa madai
Mwenyekiti wa Bunge hilo Samwel Sitta ameguza Bunge hilo kama mkutano wa chama
chake cha CCM,
1 comment
kiswahili fasaha ni-:
kuiyandama -ni kuiandama
kwaanzia- ni kuanzia
weredi- ni weledi
na mengine nimeacha so post zako nimezipenda ila kiswahili unakivunja man..!!
Post a Comment