HABARI NZITO--MCHUNGAJI MSIGWA AITETEA IKULU YA RAIS KIKWETE,AIBUKA NA KUYAVAA MAGAZETI NA KUTOA KAULI NZITO--SOMA HAPA KUJUA ZAIDI
Na Karoli
Vinsent
SIKU chache
kupita Baada ya Magazeti nchini kuituhumu ikulu ya Rais Jakaya Kikwete kwa kutoa
kibali maalum kwa Familia ya Friedkin kutoka nchini Marekani ambao
ni Marafiki wa Waziri wa Maliasili na Utalii Lazaro Nyalandu, kwa ajiri ya kuua
Wanyama 704 ikiwemo Tembo pamoja na wanyama wengine.
Naye Waziri Kivuli wa Maliasili na
Utalii,Mchungaji Peter Msigwa ameibuka na kuyavaa magazeti nchini na kusema
yanaandika Habari za Uongo.
Kauli hiyo kushangaza ya Msigwa ameitoa leo
Jijini Dar Es Salaam,wakati alipokuwa anaongea na Mwandishi wa Mtandao
huu,kuhusu Taarifa iliyoripotiwa na baadhi ya Magazeti juu ya Leseni
iliyotolewa na ikulu kwa ajiri ya kuua wanyama 704,
Ambapo msigwa alisema taarifa hizo sio
za ukweli kwani ni za uzushi mtupu kutokana na Magazeti hayo kushindwa kuweka
ushahidi wa moja kwa moja.
“Sikiliza mwandishi mimi siwezi
kuzungumzia vitu vinavyoandikwa kwenye gazeti la Fahamu,Raia Mwema pamoja na
Jamhuri kwani tumeshayazoea kuandika habari za uzushi mtupu,na hiyo nakala ya
barua wanayoitoa kwenye Gazeti sio ya ukweli tena inalengo ya kupotosha umma tu
ndio maana kambi ya upinzania tumeipotezea”alisema Msigwa.
Peter Msigwa ambaye ni mbunge wa Iringa Mjini
CHADEMA alizidi kusema kawaida ni Vema taarifa hiyo ingekuwa na ushahidi kamili
lakini wao hawakufanya hivyo na kuzidi kusema magazeti hayo yamekuwa yakipinga
kile alichokifanya yeye ikiwemo kumshinikiza waziri wa maliasili na Utalii
Lazaro nyalandu kuifungia leseni ya uwindaji,
Kwa Kampuni
ya uwindaji ya Safari.
“Mimi ningetegema magazeti hayo
yangeiga mfano wa gazeti la Gurdian limekuwa likiandika makala ya kupongeza kwa
kazi kubwa iliyofanywa ya kuifungia kampuni ya safari,kutokana na kitendo chake
cha kufanya uwindaji haramu lakini cha kushangaza magazeti hayo yamebadilika
yamekuwa yakiandika habari za uongo zenye kudanyanya Umma hizo taarifa hazina
ukweli zinafedhehesha ikulu”alizidi kusema Msigwa.
Mwandishi wa Mtandao huu alipomtajia
Nakala ya barua kutoka ikulu ambayo magazeti hayo wanaitumia kama ushahidi
,Mchungaji Msigwa alimtaka Mwandishi wa Mtandao huu amtafute Waziri nyalandu
atoe ufafanuzi kuhusu barua hiyo kutokana na
yeye kutoamini taarifa zinazoandikwa kwenye magazeti hayo.
“Mimi
ningeshtuka kama taarifa ingeandikwa kwenye Gazeti la mwananchi,Tanzania
Daima,Majira lakini unaniambia Taarifa kwenye Magazeti ya Fahamu,Jamhuri,Raia
Mwema,wakati hawana ukweli kuhusu taarifa zao,na siwezi kuwazuia kwani wamekuwa
wakibeza kazi nzuri ninayofanya mimi kwa kushirikiana na Waziri Nyalandu”
Kauli hiyo
ya Mchungaji Msigwa inazidi kuchanganya Watanzania kutokana na Taarifa
iliyolipotiwa na Magazeti nchi ambayo yamekuwa yakituhumu Ikulu ya Rais Jakaya
Kikwete kuingia kwenye Mtego mchafu ulioandaliwa na Waziri wa Maliasili Lazaro
nyalandu kutoa Leseni hiyo.
Ambapo Leseni hiyo imetoa Ruhusa kwa tembo wanane
wameruhusiwa kuuawa nchini kwa kibali maalumu cha Rais (Presidential Hunting
Licence).
Kibali hicho kilichotiwa saini na
Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Wanyamapori aliyeteuliwa na Waziri wa Maliasili na
Utalii, Lazaro Nyalandu baada ya kung’olewa katika nafasi hiyo Mkurugenzi wa
awali, Profesa Jafar Kidegesho, kimetolewa rasmi Agosti Mosi, mwaka huu na
mwisho wake wa matumizi ni kesho, Agosti 21, mwaka huu.
Katika leseni hiyo ya Rais, watu
wanane wa familia moja wameruhusiwa kuua tembo wanane kila mmoja, sambamba na
wanyama wengine ambao jumla yao ni 704. Tembo wanane maana yake ni meno ya
tembo 16.
Kwa kawaida, presidential hunting
license haitozwi malipo yoyote na hutolewa kwa malengo makuu matano. Lengo
la kwanza ni kwa ajili ya shughuli za utafiti wa kisayansi; pili, ni kwa ajili
ya shughuli za maonyesho katika makumbusho (museum); tatu ni kwa ajili
ya masuala ya elimu; nne, kwa ajili ya shughuli za kiutamaduni na tano kwa
ajili ya uwindaji ili kupata chakula pale inapojitokeza dharura ya njaa.
Hata hivyo, kinyume cha vigezo hivyo
vitano, leseni hiyo ya uwindaji ya Rais inayoruhusu kuwinda wanyama 704,
imetolewa kwa familia ya Kimarekani ya Friedkin, taifa ambalo limepiga marufuku
biashara ya meno ya tembo.
Katika leseni hiyo ya Rais,
kila mwanafamilia anaruhusiwa kuwinda jumla ya wanyama 88 kutokana na aina (species)
49 tofauti bila kulipa chochote kwa sababu ya hadhi ya leseni husika.
2 comments
najuta bila kunywa
najuta kuwa Mtanzania kwani nalewa bila kunywa
Post a Comment