Zinazobamba

HABARI NJEMA MDA HUU---RITA YAZINDUA MFUMO THABITI WENYE LENGO BORA KWA WATANZANIA--SOMA HAPA KUJA ZAIDI



Pichani katikati Afisa Mtendaji mkuu na Msajili Mkuu,wakala wa Usajili Ufilisi na Udhamini (RITA) Philip G,Saliboko Akizungumza na Waandishi wa Habari leo Jijini Dar es Salaam,(picha na Exaudi Mtei)

Na Karoli Vinsent
      WAKALA wa Usajili na ufilisi na Udhamini(RITA) kwa kushirikiana na Ofisi ya Taifa ya Takwimu(NBS) inatarajia kufanya tasmini ya mfumo wa Usajili,matukio muhimu ya Maisha na ukusanyaji wa Takwimu nchini.
            Mfumo huo ambao utatumika kuchukua taarifa muhimu za vizazi,vifo na Sababu zake,ndoa  na talaka.
Waandishi wa Habari kutoka Vyombo tofauti tofauti wakisikiliza kwa makini
             Akizungumzia Tasmini hiyo, leo Jijini Dar es Salaam wakati wa Mkutano na Waandishi Habari ,Afisa Mtendaji mkuu na Msajili Mkuu,wakala wa Usajili Ufilisi na Udhamini (RITA) Philip G,Saliboko Alisema Tasmini hiyo itafanyika kianda kwa siku kumi na tano
(15) kuanzia tarehe 15 Semptemba hadi tarehe 30 mwaka huu na itajumuisha wadau wakubwa wa Masula ya usajili kutoka wizara ,Taasisi,Idara pamoja na Vyuo na wakala Mbalimbali za Serikali.
               Ambapo aliongeza kusema Tathmini itafanywa katika ofisi za Maafisa tawala wa Wilaya,Vituo vya Tiba ,Vituo vya Polisi,nyumba vya kutunzia Maiti,makanisa na kwenye Makazi ya Wananchi ambamo matuko hayo utokea.
              Saliboko aliwataka Watanzania kutoa ushirikiana mkubwa wakati wa Zoezi hili,kwani ndio njia pekee itakayoisaidia Serikali kufanya mipango yake kikaminifu.

No comments