TAMISEMI YATOA TAARIFA NZITO KUHUSU WANAFUNZI WALIOFAHURU MASOMO YA SAYANSI,
1.0.
UTANGULIZI
Serikali inafanya juhudi mbalimbali za kukabiliana
na changamoto ya uhaba wa wataalamu katika fani za sayansi kwa kujiwekea mkakati wa kuhakikisha kuwa kila Mwanafunzi
aliyefaulu masomo ya sayansi anapangiwa tahasusi (Combination) ya masomo ya sayansi.
Katika matokeo ya
mtihani kwa mwaka 2014, inaonyesha kuwa
jumla ya wanafunzi 22,685 kati yao Wasichana 7,859 na Wavulana 14,826
wamechaguliwa kusoma tahasusi za sayansi ikilinganishwa na idadi ya wanafunzi
18,746 kati yao Wasichana 5,038 na
Wavulana 13,708 kwa mwaka 2013.
Uchaguzi wa wanafunzi kidato cha tano kwa
mwaka 2014 ulifanyika mwezi mei, 2014 na matokeo yake kutangazwa kupitia tovuti
ya OWM- TAMISEMI mwezi Juni 2014.
Tofauti na miaka mingine iliyopita, Ufaulu wa watahiniwa wa
shule kwa mwaka 2013 katika madaraja ya I -III umeongezeka kutoka watahiniwa 35,357 mwaka 2012 hadi 71,527 mwaka huu. Ufaulu huu ni zaidi ya asilimia mia
moja ya watahiniwa waliokuwa na sifa za kuendelea na masomo ya kidato cha tano
mwaka 2013.
Natoa pongezi nyingi kwa
walimu, wanafunzi,wazazi/walezi na wadau wote wa elimu kwa juhudi walizozifanya
kuwezesha ufaulu katika masomo ya sayansi kuongezeka kwa kiasi cha kuridhisha.
Matokeo haya yanakaribia
sana malengo ambayo Serikali imejiwekea
kupitia Mpango wa Matokeo Makubwa Sasa (yaani Big Results Now-BRN)
ambapo serikali ilijiwekea lengo la
kuhakikisha wanafunzi wanafaulu kwa asilimia 60 mwaka 2013. Matokeo halisi
yanaonyesha kuwa ufaulu umepanda kutoka asilimia 43 mwaka 2012 hadi asilimia
58.25 mwaka 2013.
Yapo manufaa mbalimbali
ambayo yatapatikana kutokana na ufaulu huu wa wanafunzi kwa taifa na kwa wanafunzi
husika. Kwa taifa ufaulu katika masomo ya sayansi utasaidia kupunguza uhaba wa
wataalamu katika fani mbalimbali za sayansi na pia unarahisisha kazi ya kuwapatia
wanafunzi nafasi mbalimbali za kujiendeleza katika masomo ya ngazi ya juu.
Kwa upande wa wanafunzi,
kufaulu vizuri kunawawezesha kuendelea na masomo ya juu, inasaidia kuwapatia
nafasi ya uchaguzi wa fani ambazo wangependa kusomea na pia inawajengea kujiamini
kuwa wanaweza kufanya vizuri.
2.0.
UCHAGUZI WA
WANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO
MWAKA 2014.
Wanafunzi 54,058 sawa na
asilimia 75.61 ya wanafunzi 71,527 wamechaguliwa awamu ya kwanza kujiunga
kidato cha tanoTanzania Bara kwa mwaka 2014. Aidha wanafunzi 472 wamechaguliwa
kujiunga na vyuo vya ufundi.
Uchaguzi wa wanafunzi wa kidato cha tano katika shule za
sekondari za serikali na vyuo vya ufundi kwa mwaka 2014 umefanywa kwa kuzingatia
taratibu zifuatazo:-
i.
Kila mwanafunzi kuwa na fursa ya kuchagua shule na tahasusi tano kwa
mtiririko wa vipaumbele vyake;
ii.
Mfumo wa kielectroniki umetumika ambao umeoanishwa na matokeo ya mtihani ya
watahiniwa wa kuhitimu Elimu ya Sekondari, tahasusi (combination) na shule
walizochagua kwa kutumia Selform
walizojaza wakiwa shuleni;
iii.
Mfumo wa kieletroniki umewapangia wanafunzi kwenda kidato cha tano
kulingana na sifa, nafasi kwa kila tahasusi na shule, machaguo ya wanafunzi
yaliyoko kwenye selform na mahali
anapotoka mwanafuzi;
iv.
Wanafunzi ambao wamefaulu kwa sifa ya kwenda kidato cha tano lakini
tahasusi zote tano walizochagua hazikukidhi vigezo (cut-off points) na ambao hawakujaza Selform jambo lililosababisha
mfumo kutotambua machaguo yao
(shule na tahasusi), mfumo umewachagulia
tahasusi na shule;
v.
Wanafunzi 22,685 (wasichana 7,859 na wavulana 14,826) mwaka 2014 wamechaguliwa
kusoma tahasusi za sayansi ikilinganishwa na 18,746 (wasichana 5,038 na
wavulana 13,708) mwaka 2013, uchaguzi huu uzingatia ufaulu, machaguo yao na
nafasi zilizopo katika shule husika;
vi.
Hadi 14 Julai 2014, Wanafunzi 1,518 wamebadilishiwa shule na tahasusi
kati ya 3,478 walioomba kubadilishiwa kutokana na sababu mbalimbali zikiwemo za
kiafya;
3.0.
CHANGAMOTO ZILIZOJITOKEZA
i. Wanafunzi kuomba
kubadilishiwa tahasusi na shule tofauti na zile walizochagua awali;
ii. Ufaulu wa wanafunzi
wenye sifa za kujiunga na kidato cha tano kutowiana na nafasi zilizopo;
4.0.
HITIMISHO
Serikali kwa kutambua umuhimu wa masomo ya sayansi
na mwitikio chanya uliopo sasa kwa wanafunzi kusoma masomo hayo,
imeendelea kuimarisha miundombinu ya shule kwa kutoa fedha za ujenzi,
ukamilishaji na ukarabati. Aidha, Serikali
inatarajia kufanya uchaguzi wa awamu ya pili kwa wanafunzi waliobaki kutokana na ufinyu wa nafasi za shule za
kidato cha tano, baada ya kubaini uwepo wa nafasi hizo; na tunatarajia kwamba
baadhi ya wanafunzi wenye sifa watachaguliwa kwenda kusomea ualimu.
Wanafunzi ambao wamefaulu vizuri masomo ya
sayansi na wanapenda kusoma masomo hayo wanayofursa ya kubadilisha tahasusi endapo
kwenye shule walizopangwa kupitia kwa wakuu wao wa shule. Endapo tahasusi hawafundishi kene shule hizo
wanaweza kuwasilisha maombi yao kwa Maafisa elimu Mikoa ambayo shule hizo zipo
kupitia kwa wakuu wa shule walizopangiwa ili waweze kubadilishiwa tahasusi za
sayansi kwenye shule zilizopo kwenye Mikoa husika.
Aidha, Jamii inaweza kuwasiliana na watendaji
wa Wizara na Mikoa kwa simu ambazo zinapatikana kwenye tovuti ya Ofisi ya
Waziri Mkuu – TAMISEMI . Hivyo,
naendelea kuwasisitiza watendaJi wote wa elimu hususani Wakuu wa Shule na
Maafisa Elimu Mikoa kusimamia utekelezaji wa suala hili. Lengo la Serikali ni kuwa na idadi kubwa ya
wanafunzi wanao soma masomo ya sayansi ili kuendana na malengo ya Melenia na kutekeleza
Mpango wa BRN.
Vilevile, Serikali inaendelea kusisitiza kila
mwanafunzi kwenda kuripoti shule aliyopangiwa kuanzia tarehe 10-30 Julai 2014,
orodha
ya wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na Kidato cha Tano mwaka 2014 inapatikana
katika tovuti za www.pmoralg.go.tz
na www.moe.go.tz.
IMETOLEWA
NA NDG. JUMANNE SAGINI, KATIBU MKUU OFISI YA WAZIRI MKUU TAWALA ZA MIKOA NA
SERIKALI ZA MITAA.
No comments
Post a Comment