Zinazobamba

TAARIFA KAMILI YA JESHI LA POLISI KWA WANANCHI KUHUSU SAKATA LA VIUNGO VYA BINADAM VILIVYOTUPWA JIJINI DARESALAAM HII HAPA

Jeshi la polisi kanda maalum sasa linawashikilia jumla ya watu wanane wakiwepo wafanyakazi wa taasisi ya IMTU wakihusishwa na sakata la utupwaji wa viungo vya Binadadam huko katika eneo la Bunju katika jiji la Draesalaam, kwa habari zaidi soma taarifa ya jeshi hilo hapa chini.


https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjbDeFlzVS5srl3YR6UZ6K8WmgH8ViFRIqfrh5G-sU7gVc11NWSzuI-rBwDP0w35gE-lkhoYgnAHUYncjEYkuGyy232Zm8ECxR3AXAvV11TFeETxGQpVU2eGWJk0SyGzMhr9PJQQpRrJrp9/s1600/3.jpg
Kamishina wa polisi kanda maalum ya Daresalaam akitoa ufafanuzi juu ya viungo vya binadam vilitupwa hapa jijini Daresalaam, Kamata kova amesema taarifa za awali zinaonyesha viungo hivyo vimetoka katika hospitali na chuo Cha IMTU hata hivyo jeshi hilo limeunda tume kuchunguza habari hiyo ili kubaini kwa nini viungo hivyo vya binadam kutupwa eneo hilo, 


Mabaki ya miili iliyotupwa eneo la Bunju Dar es Salaam







                                                JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
                             WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI
JESHI LA POLISI TANZANIA



PRESS RELEASE
22/07/2014

WATU WANANE WAKIWEMO MADAKTARI WASHIKILIWA NA KUHOJIWA NA JESHI LA POLISI KUTOKANA NA KUTUPWA VIUNGO VYA BINADAMU MAENEO YA BONDE LA MBWENI MPIJI ENEO LA BUNJU

Jeshi la Polisi Kanda Maalum Dar es Salaam linawashikilia watu wanane na kuwahoji kuhusu tukio la kupatina na viungo vya binadamu vilivyogundulika katika maeneo ya bonde la Mbweni Mpiji ambapo mifuko ya plastiki ipatayo 85 yenye mabaki ya viungo vya binadamu yaligundulika.  Polisi walipata taarifa 21/07/2014 jioni kutoka kwa wasamaria wema na ndipo jopo la wapelelezi likiongozwa na Mkuu wa Polisi Mkoa wa Kipolisi Kinondoni ACP. Camilius Wambura walifika hapo majira ya saa 1.00 usiku.

Walipofika katika tukio waligundua mifuko ipatayo 85 mieusi yenye viungo vya aina mbali mbali vya binadamu kama vile Vichwa, Miguu, Mikono, Mioyo, mapafu, vifua na mifupa ya aina mbali mbali ya binadamu.  Viungo hivyo havikuwa na uvundo au harufu ya aina yoyote na vilionekana kwamba vimekaushwa na kukakamaa. Katika eneo hilo pia vilikutwa vifaa vinavyotumika hospitali kama vile mipira ya kuvaa mikononi (gloves) mifuko miwili iliyotumika ,nguo maalum (apron) zipatazo 20 na karatasi mbili zenye maswali ya kujibu. 

Wananchi wasiopungua 1,000 walifika katika eneo hilo la tukio lakini hakuna aliyekuwa na taarifa sahihi.  Viungo hivyo vilichukuliwa na kupelekwa hospitali ya Muhimbili kwa uchunguzi zaidi.  Aidha jopo la Wapelelezi chini ya Mkuu wa Upelelezi Kanda Maalum ACP. Japhari Mohamed walianza uchunguzi mara moja kwa kusaidiana na Daktari wa Jeshi la Polisi anayehusika na uchunguzi wa miili ya binadamu (Forensic Doctor) ambaye kwa pamoja walishirikiana na madaktari wengine kutoka hospitali wa Taifa Muhimbili. 



Hatimaye uchunguzi wa kina ulibaini kwamba viungo hivyo kwa mara ya mwisho vilikuwa katika Maabara ya Chuo Kikuu Madaktari IMTU jijini D’Salaam.  Baada ya kugundulika hivyo Polisi wamewakamata na sasa wanaendelea kuwahoji watu wanane ambao wanasadikiwa kuhusika na miili hiyo ikiwa ni pamoja na baadhi ya  madaktari wa IMTU. IMTU (International Medical and Technolegical Univester) ni chuo Kikuu cha Madaktari ambacho pia hufanya mafunzo ya udakitari kwa vitendo (practical).  Jeshi la Polisi Kanda Maalum litamuhusisha Mkemia Mkuu wa Serikali na hatimaye mara baada ya kukamilika kwa uchunguzi jalada litapelekwa kwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali kwa hatua zake ili sheria ichukue mkondo wake.







S. H. KOVA

KAMISHNA WA POLISI KANDA MAALUM

DAR ES SALAAM


















No comments