Zinazobamba

NI HUZUNI----HALI YA MSANII BAHATI BUKUKU YAZIDI KUWA MBAYA SANA,SASA HAWEZI KUKAA WALA KUTEMBEA SOMA HAPA KUJUA KWANINI



 
Pichani ni Msanii wa Nyimbo za Injiri Bahati Bukuku akiwa amelezwa,

Na Karoli Vinsent
HALI ya Msanii Hodari wa Nyimbo za Injiri Nchini Tanzania Bahati Bukuku inazidi kuwa mbaya,sasa kinachoitajika ni Maombi na sara  kutoka kwa Watanzania ndio itakayoweza kumwokoa Msanii huyo wa Injiri,Mtadano umeambiwa.
         Bahati Bukuku,ambaye alipata ajari mbaya ya Gari iliyotokea usiku wa kuamkia Jumapili  iliyopita kwenye eneo la Ranchi ya Narco wilayani Kongwa  Mkoani Dodoma m,ajira ya saa tisa usiku wakati alipokuwa anakwenda Mkoani Shinyanga,Kahama kwenye mkutano wa Injiri ambapo ajari ndiyo iliomleta matatizo makubwa.
            Akizungumza na Mwandishi wa Mtandao kwa Njia  ya Simu Rafiki wa karibu wa bahati Bukuku,ambaye akutaka kutaja Jina kwenye Mtandao huu kwa kusema yeye sio msemaji wa Familiya Bukuku alisema kwa sasa hali ya Bahati bukuku inazidi kuwa mbaya sana na  sasa kinachoitajika ni sara na Maombi tu.

      “Da leo nimeoka kumwangalia Hospitari yaani da hali ya Rafiki yangu Bahati Bukuku ni mbaya sana na kinachoitajika sahivi ni maombi tu,maana ukimwangalia mpaka unapatwa na huruma sana tena unapata maswali ya kujiuliza huyo ndio msanii mwenye afya tele juzi tu?”alihoji mpashaji huyoHabari.
              Pichani ni gari alikuwa akilitumia Msanii Bahati Bukuku
 Mwandishi wa Mtanda huu alipomtaka Rafiki huyo ataje kitu gani kinachopelea hali yake bahati bukuku kuwa mbaya,
        “Bahati ameumia sana kwenye kiuno na ukimwangalia utajua Kiuno kimevunjika na sehemu zengine ikiwemo Shingo hawezi kukaa wala kutembea yeye amekuwa mtu wa Kulala tu,na kinachoitajika sahivi ni sara tu sio kitu kengine maana uwezekano wa kupona ni mdogo sana”alisema mtoa huyo taarifa.
             Msanii Bahati Bukuku,ambaye anatamba nyimbo kadhaa ikiwemo Dunia haina Huruma,Maamuzi pamoja na Majaribu ambapo katika Ajari hiyo  Dereva wa Gari aliyokuwa anasafilia haina ya Toyota Nadia lenye namba za usajili T 7945 Edsoni Mwakabungu “EDY” Miaka 31 ambaye ameumia Vibaya sana na Vidole na pia hawezi kutembea kabisa
            Watu wengine waliokuwemo kwenye Ajari hiyo  ni Wacheza shoo wa Bahati Bukuku Franki Muha (20) na mwenzake kwa Jina halikupatikana mala moja.
       Naye Bahati Bukuku alinikuliwa na Mtandao mmoja wa Habari huku akisema kwa shida sana alisema kwa sasa hali yake ni mbaya sana na kuwataka watanzania kumwombea ili apone na aje kuendelea na kazi yake ya kuendeza Injiri.
             Msanii huyo ambaye ni Mwenyeji Mkoani Mbeya kwa sasa bado amelazwa Hospitari ya Taifa ya Muhimbili Jijini Dar es Salaam .

No comments