Zinazobamba

MATUSI, KEBEHI DHIDI YA BABA WA TAIFA MWL. JURIUS KAMBARAGE NYERER SASA YACHUKUA SURA MPYA


Mtoto wa baba wa taifa hili, Mwl Jurius Kambarage nyerere Makongoro Nyere (mwenye suti nyeusi)akipokea ugeni toka umoja wa vijana CCM, uliotembelea nyumbani kwa muasisi wa taifa hili kwenda kumuona bibi yao Mama maria Nyere na kumueleza masikitiko yao juu ya hatua za baadhi ya viongozi tena ndani ya bunge kumtusi baba wa taifa, wamesema hakika wanasikitishwa sana na viendo ovu vya kumtusi baba wa taifa.Alivalia shati la kijani ni mzee wetu Kifupa.

Makongoro akiwa mwenye nyuso za furaha baada ya kupokea ugeni huo toka kwa umoja wa vijana wa ccm.

Baada ya kuwapokea alipata fursa ya kuwaingiza ndani ili waseme walitaka kusema kwa bibi yao

Mwenyekiti wa UVCCM mkoa wa Daresalaam akitoa salam zake kwa wenyeji nyumbani kwa mjane, mama Maria nyerere

Umoja huo ulikuja na miti ili kupanda katika mashamba yaliyo ndani mwa nyumba ya mama Maria nyerere, Huyu ni mmoja aliyebeba miti hiyo


Makongoro Nyerere akiwa sambamba na Mjane wa Baba wa Taifa, Mama Maria Nyerere alipoenda kumtoa ndani ili azungumze na wajukuu zake waliomtembela nyumbani kwake.

Kiongozi wa Jumuiko La vijana Bw. Mohammedi Nyundo, Akimpa tamko la Umoja wa vijana UVCCM  mama maria nyerer baada ya kulisoma kwa niaba ya umoja huo. Tamko hilo limelaani vikali hatua za kumtusi baba wa taifa na kumshushia heshima yake.

Bibi, akizungumza na wajukuu wake nyumbani kwake, Mama malia nyerere amewasifu hatua ambayo vijana wa ccm wameionyeshwa na kusema wanatakiwa hata kuzunguka nchi nzima kuwaeleza watanzania ukweli na umuhimu wa kuthamini wazee wetu, AMESEMA KUTUSI WAZEE WETU NI SAWA NA KULAANIWA. Hata hivyo vijana hao wamemuhakikishia bibi kuwa wataenda na kwa mjane Mama Abeid AMAN Karume ili kwenda kupeleka masikitiko yao na jinsi walivyogusa na hatua ya watu kutukana waasisi wa taifa lao tena wakitumia bunge letu tukufu.


Makongoro Nyerere akishiriki zoezi la upandaji miti kwa niaba ya Bibi, mama Maria nyerere.


Umoja wa vijana wa CCM (UVCCM) tamko lao la kuulaani vitendo viovu vya baadhi ya watu kumtuhumu, kumkebehi na kumtukana baba wa taifa , Mwl. Jurius Kambarage Nyerere mapema hii leo nyumbani kwa mjane Mama  Maria Nyerer,
Tamko hilo limekuja kufuatia kampeni kambambe ambazo zinaendeshwa na wapinga amani na wale wanaojifanya hawaoni kazi nzuri iliyofanywa na Baba wa taifa, ambao hivi karibuni wamekuwa wakinukuliwa wakitoa maneneo ya kashifa dhidi ya Baba wa Taifa,,
Akizungumza nyumbani kwa mjane Mama Maria nyerer, Kiongozi wa Jumuiko la Vijana wazalendo, na mwenyekiti wa vijana mkoa wa Pwani, Bw. Mohammedi Nyumbo,amesema kumekuwepo na  kampeni yenye nia ovu iliyoasisiwa hivi karibuni ya kuharibu taswira na heshima ya baba wa taifa katika jamii ya kitanzania na kimataifa.,
Amesema kampeni hiyo inayoendeshwa na vibaraka wan chi za magharibi na ulaya, Wazandiki na maadui wa amani ya Tanzania imeendelea kusambaa kwa kasi na kwa gharama kubwa, hatua inayonyesha  kuharikisha mchakato wa  kuharibu taswira ya baba wa taifa,
Amesema kwa kutambua mchango wa baba wa taifa kama muasisi wa taifa hili,mpigania uhuru shupavu, shujaa aliyekuwa na mapenzi  ya dhati na taifa lake, umoja huo umeamua kuukumbusha  umma wa kitanzania juu ya mchango  uliotukuka wa baba wa taifa katika taifa hili na kuhamasisha vijana kuenzi  kwa vitendo moyo wa kujituma, weledi na busara za mwalimu ili kuweza kuwa na taifa lenye misingi  ya kuheshimu wazee wetu.
Aidha katika hatua nyingine Umoja huo wa vijana umesikitishwa na vitendo vya bunge la jamuhuri ya muungano wa Tanznaia kugeuka kuwa uwanja wa matusi wa kumtukana baba wa Taifa, hakika imewafedhehesha sana,
Nazani imefika wakati sasa kwa bunge tukufu la Tanzania, kudhibiti na kuondoa kinga yake kwa wale wote ambao kwa ujinga na kutumika wameamua kuanzisha kuendesha  kampeni ya kutia doa taswira ya BABA wa taifa hili tukufu

No comments