Zinazobamba

taarifa ya tigo kwa waandishi wa habari juu ya uzinduzi wa mpango salama




TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
 
Tigo yadhamini mpango wa kupunguza ajali za bodaboda nchini
Dar es Salaam, 18 Machi 2014 – Tigo Tanzania imetangaza kushirikiana na taasisi ya usalama wa pikipiki nchini katika kuzindua Mpango wa Huduma Salama ya Usafiri wa Bodaboda Kitaifa itakayofanyika mjini Dodoma, 23 Machi, 2014.
Akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, iliyowashirikisha pia wakala wa usalama wa pikipiki nchini (TAMOSA), Meneja Mawasiliano wa Tigo, John Wanyancha, alisema kwamba udhamini wa Tigo katika mpango huo wa kitaifa wa usalama wa bodaboda nchini ni ishara ya kwamba kampuni hiyo ya simu inajali na kufuatilia kwa karibu kuhusu masuala ya usalama barabarani nchini.
 “Wote ni mashuhuda wa jinsi biashara hii ya pikipiki ilivyoweza kushamiri ndani ya muda mfupi nchini. Kupitia bodaboda na bajaji vijana wetu wameweza kujiajiri wenyewe na kuweza kujipatia kipato kinachowasaidia kumudu maisha,” alisema Wanyancha.
 “Lakini kila kitu huja na changamoto zake, na katika hili suala la ajali barabarani limekuwa dosari kubwa. Kama kampuni, tuliamini kwamba hii itakuwa fursa nzuri kwa sisi kama wadau kujaribu kuhamasisha kuhusu usalama barabarani kwa ajili ya kusaidia kupunguza idadi ya ajali zinazotokea huku tukihakikisha kwamba sekta hii inaendelea kuwa chachu ya ajira kwa vijana nchini,” alisema.

Kutokana na maelezo ya Mratibu wa Matukio kutoka TAMOSA, Kizito Msangya, alisema kwamba uzinduzi wa mpango huo wa usalama utafanyika kwa njia ya maandamo ya amani kutoka ofisi ya Mkuu wa Mkoa mpaka Uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma ambapo Waziri Mkuu Mizengo Peter Pinda ndio atakuwa mgeni rasmi.
“Tunatarajia mamia ya wamiliki na waendesha pikipiki kutoka nchini kote kufika katika tukio hili. Ukiondoa mbali na Mheshimiwa Pinda, pia tunatarajia Waziri wa Uchukuzi Dk. Harrison Mwakyembe, wabunge pamoja na mamlaka za usalama barabarani kushiriki katika uzinduzi huu,” alisema Msangya.
Ripoti za Polisi zinaonyesha kuwa kumekuwa na ongezeko la matukio  264 ya ajali barabarani   kwa mwaka 2013 sawa na asilimia 1.1  tofauti na mwaka 2012  ambapo  matukio yalikuwa 23,578.
Takwimu pia zinaonyesha kuwa walioathirika  zaidi na ajali za barabarani  kwa mwaka 2013 ni waenda kwa miguu, abiria, waendesha pikipiki, wapanda baiskeli, madereva  pamoja na wasukuma mikokoteni. Ambapo kati ya makundi hayo, ajali za pikipiki zimeongoza  kwa ajali nyingi, kwa mwaka 2013 ajali zilikuwa 6,831 sawa na ongezeko la asilimia 18.5 ya ajali 5,763 zilizotokea mwaka juzi.
Mwisho.
Kuhusu Tigo:

Tigo ni mtandao wa kwanza wa simu za mkononi nchini Tanzania. Ilianza shughuli mwaka 1994 na inapatikana katika mikoa thelathini (30) Tanzania bara na visiwani.

Lengo la Tigo ni kuwa mtandao unaoongoza kwa kutoa huduma bora na za ubunifu Tanzania kwa wateja wake wote ambazo zinaendana na mahitaji yao kuanzia huduma za sauti za bei nafuu, vifurushi vya intaneti vyenye kasi kubwa na huduma bora za fedha za simu za mkononi kupitia Tigo Pesa.

Tigo ni sehemu ya kampuni kubwa ya Millicom ambayo ni ya unafuu wa huduma na inapatikana kirahisi  kwa zaidi ya wateja milioni 47 katika masoko 13 barani Afrika na Amerika ya Kusini.

"Tabasamu upo na Tigo." Kwa taarifa zaidi tembelea www.tigo.co.tz  
Au wasiliana na: John Wanyancha – Meneja Mawasiliano Tigo Simu: +255 658 123 089 john.wanyancha@tigo.co.tz

No comments