Zinazobamba

KIZENGA: DUDU LINALOITAFUNA NIT/DIT, WANAFUNZI WACHEKELEA WASEMA MAISHA SASA MTEREMKO, NIT BILA KUSOMA INAWEZEKANA, SOMA HAPAAA

http://i.dailymail.co.uk/i/pix/2013/10/28/article-2478138-1508B29A000005DC-249_634x397.jpgImeelezwa kuwa chuo cha Taifa cha usafirishaji na kile cha chuo cha Technologia cha Dresalam kwa sasa vimekubwa na dudu baya liitwalo Kizenga ambapo kila mwanafunzi sasa wameacha kusoma na kujikita katika mazingira ya kuandaa kizenga

Wakizungumza na fullhabari mapema mwishoni mwa wiki hii, wanafunzi ambao walioonyeshwa kukerwa na kitendo cha baadhi ya wanafunzi kutumia kizenga, wamesema sasa katika vyuo hivyo kunanuka vizenga katika ngazi zote za masomo

Wamesema sasa hali hiyo imeeota mizizi na kwamba hata wale ambao walikuwa na moyo safi wa kujisomea sasa wamebadili tabia na kuanza kuiga tabia za wanafunzi wenzao ambao wanaonekana kupata alama kubwa katika mitihani yao huku wale wanaotegemea vichwa vyao wakiangukia pua

WAKIZUNGUMZIA namna ya wanafunzi hao wanavyoweza kutumia zana hizo saidizi zilizopachikwa jina la Kizenga katika vyuo hivyo, Wanafunzi hao wamesema, kutokana na usimamizi mdogo wa walimu huku darasa kuwa na idadi kubwa ya wanafunzi ndio sababu kubwa ya wanafunzi kuweza kutumia Kizenga katika mitihani mbalimbali

"Ndugu mwandishi hakuna usimamizi kabisa unakuta Darasa zima lenye wanafunzi mia tatu linasimamiwa na mwalimu wa somo peke yake, inafika wakati anashindwa kulimiki darasa kutokana na ukubwa wa darasa, tunazani hii siyo haki hata kidogo, lazima wenye dhamana wafanye kitu katika kunasua tatizo hili kwa sasa"walisema
Katika chuo cha DIT imebainika wanafunzi kutuia vizenga, na kwamba kila mwanafunzi sasa anaona njia nyepesi ya kufaulu mitihani ni kutumia kizenga,
Unakuta mwanafunzi kila mfuko ameweka Topic ya somo kwa hiyo akifika katika mtihani ni kuingiza mikono katika mfuko wenye jibu la swali lake,

KWA HABARI ZAIDI FULLHABARI ITAKULETEA MAJIBU YA WENYE MAMLAKA KWA SASA MPAKA TUNAENDA MITAMBONI TUMESHINDWA KUWASILIANA NAO, KWA SABABU ZILIZO NJE YA UWEZO WETU

No comments