Zinazobamba

WASANII WAKABIZIWA NYUMBA MKURANGA



Na Kasali Mgawe
Vifijo na nderemo vilisikika kwa wingi wilayani mkuranga mkoa wa pwani baada ya kufanyika tukio kubwa la kuwakabizi nyumba wasanii 38 wanachama wa mtandao wa wasanii Tanzania (SHIWATA)

Tukio hilo lililovutia wakazi wa eneo la mkuranga na vijiji vya jirani liliweza kuwakutanisha wasanii ,waandishi wa habari na wanamichezo ambao kwa pamoja walipata burudani mbalimbali za ngoma maigizo na sarakasi.

MGENI RAMSI AFISA TRAFA YA SHUNGUBWENI CLEMENT MUYA AKITOA HUTUBA KATIKA SHEREHE HIYO ALIMUWAKILISHA MKUU WAWILAYA YA MKURANGA

MMOJA WA WASANII WALIOKABIDHIWA NYUMBA AKIONYESHA CHETI CHAKO CHA UTAMBUZI

MWENYEKITI WA SHIWATA KASIMU TAALIBU AKITOA HUTUBA KATIKA SHEREHE HIZO

MKUU WA WILAYA YA MKURANGA MSTAAFU AKITOA HENRY CLEMENSE AKIZUNGUMZA KATIKA SHEREHE HIZO

NYUMBA MOJA WAPO YA KISASA ILIYOKABIDHIWA KATIKA SHEREHE HIZO

WASANII WALIOKABIDHIWA NYUMBA ZAO WAKIWA KATIKA PICHA YA PAMOJA NA VIONGOZI WA SHIWATA NA MGENI RASMI ALIYEMUAKILISHA MKUU WA WILYA MKURANGA

BAADHI YA NYUMBA ZILIZOKABIDHIWA KWA WASANII WANACHAMA WA SHIWATA KATIKA KIJIJI CHA MWANZEGA MKURANGA

MCHEZAJI WA ZAMANI WA TAIFA STARS JERRY MTAGWA AKIKABIDHIWA CHETI NA NYUMBA KUTOKA KWA MGENI RASMI

MMOJA WA WASANII AKIKABISHIWA NYUMBA YAKE  NA CHETI CHA UTAMBUZI NA MGENI RASMI 

BAADHI YA WASANII WAKITUM,BUIZA KATIKA SHEREHE HIZO

Akizungumza katika tukio hilo afisa tarafa ya shungubweni Mkuranga ndugu Clement Muya ambaye alimuwakilisha mkuu wa wilaya ya mkuranga alisema kuwa SHIWATA imefanya jambo kubwa kwa wasanii kwa kuweza kuwaunganisha na kuchukua maeneo ili waweze kujenga na kufanya shughuli za kilimo

Bwana Muya aliongeza kuwa ni muhimu kwa wasanii wajitambue  na kujiweka mbali na mambo 
yasiyofaa katika jamii kama utumiaji wa dawa za kulevya na wajiunge kwenye mtandao wa wasanii wenye lengo la kusaida wasanii hapa nchini kuwa na maisha na makazi bora.

Wakati huo mkuu wa wilaya ya mkuranga mstaafu Henry Omuya Clemense  ambaye alikuwa mgeni mualikwa katika sherehe hiyo alisema kuwa SHIWATA imeweza  kutekeleza mpango wake wa kuwaunganisha wasanii na kuwajengea misingi mizuri ya maisha kwa kuwa na makazi bora.

Mkuu wa wilaya huyo mstaafu aliongeza kuwa SHIWATA  imeleta mabadiliko kwa wakazi wa mkuranga kwani kwa kupita mipango yao huduma za jamii zitaongezeka kama vile huduma za  maji na shule katika eneo hilo.

Akizungumza wakati wa kumkaribisha mgeni rasmi mwenyekiti wa mtandao wa wasanii tanzania (SHIWATA) mwalimu Cassim Talib alisema   wamejipanga kuwasaidia wasanii kuweza kutoka katika wimbi la umasikini kwa kuwaandalia mazingira mazuri ya maisha yao.

Mwenyeki ti huyo alisema kuwa wanachama zaidi ya 200 wamechangia ujenzi wa nyumba hizo na wanachama 38 ndiyo walimaliza michango yao na kuweza kukabidhiwa nyumba hizo zenye thamani tofauti kutokana na uchangiaji wake.

Akitoa shukrani kwa niaba ya wasanii wenzake waliokabidhiwa nyumba hizo ndugu Jerry Mtagwa ambaye ni mchezaji wa zamani wa Taifa Stars alisema kuwa anashukuru sana SHIWATA kwa kumuwezesha kuweza kumiliki nyumba hiyo kwani itakuwa ni msaada mkubwa kwa yeye familia yake.

Mtwagwa ametoa wito kwa wasanii wengine wajiunge na SHIWATA  ni kimbilio la wasanii na itakuwa msaada wa mkubwa kwa maisha ya sasa na ya baadae kwani asalimia kubwa wanaishi katika dimbwi kubwa la umasikini.



No comments