Zinazobamba

SEKRETARIETI YA AJIRA YAWAFUNDA WANAFUNZI WALIOPO MASHULENI, YASEMA NI BUSARA KUOMBA USHAURI KABLA HUJAOMBA FANI KUJIUNGA CHUONI


               
Selemani Ahamadi
Daresalaam
Wanafunzi waliopo mashuleni wameshauriwa kujiunga na kozi za masomo ya Afya,Elimu na Kilimo kama kweli wanataka kuajiriwa moja kwa moja serikalini kwani kwa sasa sekta hiyo kuna uhaba mkubwa sana wa wafanyakazi wake hapa nchini,

Akizungumza na wanahabari hivi karibuni jijini Daresalaam ,Msemaji na mkuu wa kitengo cha mawasiliano serikalini,ofisi ya rais sekretarieti ya ajira katika utumishi wa umma Bi. Riziki Abraham amesema kwa sasa sekta ya afya,elimu na kilimo bado zinamahitaji makubwa sana hivyo wanafunzi wanaootaka kujiunga na masongo ngazi ya chuo ni vema wakajikita katika fani hizo ili kuondoa usumbufu wa kupata ajira
MSEMAJI NA MKUU WA KITENGO CHA MAWASILIANO SELIKALINI,OFISI YA RAIS SEKRETARIETI YA AJIRA KATIKA UTUMISHI WA UMMA AKIFAFANUA JAMBO KWA WANAHABARI JUU YA UMUHIMU WA FANI ZA AFYA,ELIMU NA KILIMO KWA SASA.

WANAHABARI WAKIWA KAZINI, 



Aidha Bi. Abraham ameongeza kusema kuwa sekretarieti ya ajira wako katika mpango wa kuwawezesha waombaji wa fursa za ajira kuwasilisha maombi yao ya kazi kwa mumo wa kielektroniki (e-application) kwa nafasi wazi zitakazokuwa zikitangazwa katika utumishi wa umma ili kurahisisha kupunguza mlolongo wa uendeshaji wa mchakato wa ajira

Vilevile msemaji huyo wa sekretarieti ya ajira amewataka wananchi kuondoa fikra potofu ya kuwa ni lazima uwe na mtu wa karibu ili maombi yako yafanyiwe haki, kwani  uendeshaji wa mchakato wa ajira katika utumishi wa umma ni wa wazi na wa haki

HAPA AKIENDELEA KUTOA UFAFANUZI JUU YA MAWAZO POTOFU YALIJAA VICHWANI MWA WADAU KUWA NI LAZIMA UWE NA MTU WA KUKUBEBA ILI UPATE AJIRA,AMESEMA HAKUNA KITU HICHO
“Nataka niwaambie wanaomba fulsa ya kuajiriwa lazima wahakikishe wamefika viwango vinavyotakiwa na nafasi inayoombwa vinginevyo huwezi kupata nafasi hiyo kwani vigezo na mashariti lazima vifuatwe, hakuna kubebana katika mchakato mzima” Aliongeza Bi. Abraham


Katika hatua nyingine sekretarieti ya utumishi wa umma imetangaza idadi ya watu waliofoji vyeti mbalimbali wakati wa kuomba nafasi wazi ya ajira na kwamba mpaka sasa jumla ya vyeti 677 vya kughushi vimekamatwa ambapo wahusika wa vyeti hivyo wanadai kuvipata katika taasisis za RITA,VETA na NECTA

Watu hao wameondolewa katika mchakato na kwamba hatua za kisheria zitafuata ili kutoa funzo kwa wengine wasiendelee na tabia kama hizo

No comments