Zinazobamba

PINDA APOKEA SHEHENA YA KWANZA YA MABOMBA YA GESI,ASEMA SASA KAZI IMEANZA RASMI, ATAKA WADAU,WANAHARAKATI KUUNGA MKONO DHAMIRA YA SELIKARI



                    
WAZIRI mkuu wa Tanzania Mh. Mizengo Pinda amepokea shehena ya kwanza ya mabomba ya kusafirishia gesi toka mkoa wa Mtwara hadi Kinyerezi jijini Darealaam ujenzi utakaokamilika baada ya miezi kumi na minane
WAZIRI MKUU WA TZNANIA AKITOA NENO KWA WANANCHI WALIOHUDHULIA KATIKA MAPOKEZI YA SHEHENA YA KWANZA YA MABOMBA TOKA NCHINI CHINA,JUMLA YA MABOMBA 3500 YALIWASILI KATIKA BANDALI YA DARESALAA

MABOMBA KABLA HAYAJASHUSHWA KATIKA MELI,MENGINE YAKIWA YAMESHIKWA NA FORKLIFT TAYARI KWA KUWEKA KATIKA MALOLI YALIOWEKA TAYARI KWA KUSAFIRISHA MABOMBA HAO KWENDA HUKO MTWARA

MABOMBA YAKISHUSHWA TAYARI KWA SAFARI YA KWENDA MTWARA

HAPA YAKIWA YAMESHAPAKIWA KATIKA GARI MAALUM TAYARI KWA SAFARI

Akipokea shehena hiyo ya mabomba toka nchini China Pinda amesema wadau wote kwa pamoja ni vema tukawa watoa elimu kwa wenzetu ambao kwa namna moja ama nyingine bado hawana uwelewa mzuri wa umuhimu wa kusafirisha gesi hiyo toka Mtwara kwenda Jijini Daresalaam

Pinda ameongeza kusema kuwa mradi huu unategemewa kuongeza ajira kwa Watanzania na kwamba ukikamilika utatoa uhakika wa nishati ya umeme na hivyo kuliondoa Taifa katika giza ambalo limekuwa likiisumbua taifa kwa muda mrefu

Waziri wa nishati na madini Professa sospeter Muhongo Akifafanua jambo juu ya faida zitakazopatiakani pindi ujenzi wa mabomba hayo yatakapo kamilika
Shehena hiyo imeingiza jumla ya mabomba elf tatu mia tano (3500) ambayo yanaweza kujenga kilomita 40 toka mkoani Mtwara,

Naye mkurugenzi mtendaji wa TPDC  akimkaribisha mgeni rasmi katika mapokei hayo ya Mabomba ya kusafirisha gesi, amesema  huu ni mwanzo lakini zoezi kama hili litafuatia huko mkoani Mtwara ambapo pia Waziri mkuu atakuwepo kupokea shehena hiyo ya pili hivi karibuni

MKURUGENZI MTENDAJI WA TPDC BW. YONNA KILLAGANE AKIFAFANUA JAMBO KATIKA MAPOKEZI YA SHEHENA YA KWANZA YA MABOMBA YA KUSAFIRISHA GESI TOKA MTWARA HA DSM
Mradi huo wa kusafirisha gesi toka Mtwara utaighalimu serikali jumla ya bilion 1.2 za marekani ambazo ni feha zetu tulizokopa toka benki ya Exim ya China yenye riba nafuu, na hivyo kuondoa dhana iliyojengeka kuwa mabomba haya ni ya watu wa china

No comments