Zinazobamba

Mbeto : Sera za CCM msingi wa mageuzi ya maendeleo Zanzibar


Na Mwandishi   Wetu, Zanzibar 

Chama Cha Mapinduzi (CCM)  kimesema sera zake  zimejenga msingi wa  uchumi imara  Zanzibar  na kubadilisha aina ya mfumo wa  maisha  kwa  miaka minne iliopita .

Pia  chama hicho  kimeahidi kutekeleza tafsiri ya  Siasa kutumikia Uchumi , Siasa  safi na Uongozi bora, utakaokuza ustawi na maisha bora zaidi  miaka mitano ijayo .

Hayo yameelezwa na   Katibu  wa Kamati  Maalum  ya NEC  idara ya Itikadi  Uenezi na Mafunzo  ,Khamis Mbeto  Khamis , akiwa katika Kisiwa cha Tumbatu , Mkoa wa Kaskazini Unguja katika zoezi la uandikishaji  wapiga kura. 

Mbeto  alisema Rais  wa Zanzibar Dk Hussein Mwinyi  na serikali yake ,  amejipanga kimkakati  ili  kuacha alama ya uongozi na utumishi bora  kwa Zanzibar  na watu wake  .

Alisema katika awamu ya kwanza minne iliopita , SMZ  imejikita  zaidi katika  kusimamia mpango ya mkakati wa ujenzi wa miundombinu ya maendeleo  , kuinua huduma za kisekta na uwekaji bora wa mifumo ya kiutendaji Serikalini  kwa  viwango stahili .

" Wanasiasa hawa hawa   wanaodhihaki  utendaji  wa  smz  majukwani na kudhani  ni simulizi,  wajiandae kuaibika. Watashuhudia mabadiliko  ya kimaendeleo yatakayoacha alama kwa miaka mingi ijayo  Unguja na P emba " Alisema Mbeto .

Kadhalika ,alisema wanaokosoa leo  kwa jazba za kisiasa na kudai  hakuna  kilichofanyika , siku moja  watakakuwa wa kwanza kusifu  Zanzibar itakavyochupa kimaendeleo " Alisema Mbeto 

Aidha alisema Rais Dk Mwinyi  hatakatishwa tamaa kwa maneno ya udaku wa  kisiasa , utapitapi  wa vibaraka  wenye uzezeta unaowafanya kupiga vita  juhudi za maendeleo  .

'Sera  za CCM miaka mitano ijayo  2025 -2030  zitaibadili Zanzibar na kuipandisha  chati  kwa kiwango cha juu . Wanasiasa  uchwara wataifumba midomo yao  . Hapo ndipo kila mmoja atakapotafuta  alipomfunga punda wake"  Alisisitiza Mbeto. 

Katibu  huyo Mwenezi   alikuwa ajibu baadhi ya maswali   ya waandishi  kwa anavyoutazama uongozi wa  Rais  Dkt Mwinyi  miaka mitano ijayo ikiwa atashika tena  madaraka .

"Kwanza  nikuhakikishieni Rais Dk Mwinyi hatashindwa  uchaguzi.  Hata wapinzani  wetu hilo  wanalijua  . Tunajivunia ufanisi wa  kazi na utelelezaji wa sera zetu  toka mwaka 2020 hadi oktoba Mwaka huu " Alisema Mbeto  kwa kujiamini.

Mwenezi huyo  pia amezisifu Kamati za Ulinzi na Usalama  Wilaya za Kaskazini ' A' na 'B" Mkoa ya Kaskazini  Unguja  kwa kusimamia  usalama na kuhakikisha kila aliyekidhi vigezo vya sheria amepata nafasi ya kujiandikisha.

Hakuna maoni