Zinazobamba

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI ALEXANDER PASTORY MNYETI AZINDUA RASMI MRADI WA "THE BAHARI ACCELERATOR"

Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mh.Alexander Pastory Mnyeti,amezindua rasmi The BAHARI Accelerator,jukwaa linalolenga kuendeleza ubunifu na maendeleo endelevu kwa kugeuza tafiti za kisayansi kuwa fursa za kibiashara katika uchumi wa buluu wa Tanzania.

Naibu Waziri Mnyeti amezindua Mradi huo Februari 24,2025 Jijini Dar es salaam  wakati wa  maadhimisho ya wiki ya Bahari yanayofanyika kwa siku tano katika hotel ya Ramada Jijini humo.

Mradi huu upo chini ya Taasisi ya Utafiti wa Uvuvi Tanzania (TAFIRI) kupitia Wizara ya Mifugo na Uvuvi, kwa kushirikiana na Twiga Connect Platform kama washirika wa utekelezaji na washauri wa masuala ya uwekezaji na biashara.

Aidha Mradi huo umelenga kutoa Fursa kwa Watafiti, Wajasiriamali Wawekezaji kwenye uchumi wa buluu endelevu pamoja na kubadili Sayansi kuwa biashara.

Hata hivyo Mnyeti emesema kuwa wavuvi na wananchi kwa ujumla watapatiwa elimu na nyezo kwaajili kukuza uchumi wa buluu kwa kutumia bahari.

"Lengo kuu la The  BAHARI Accelerator ni kuendeleza ubunifu na maendeleo endelevu kupitia biashara za kisayansi kwa kugeuza tafiti za kisayansi kuwa fursa za kibiashara katika uchumi wa buluu wa Tanzania."amesema Nakuongeza kuwa Mhe. Rais Dkt.Samia ameweka nguvu kubwa kwenye uchumi wa Buluu kwa kuanza na elimu kwa wavuvi na wananchi wetu, Elimu hii itawafanya kujua nini kilichopo kwenye uchumi wa buluu” amesema Naibu Waziri huyo wa Mifugo na Uvuvi.

Aidha ameongeza  kuwa jitihada anazoendelea kufanya  mhe.Rais Dkt. Samia Suluhu Hassani ni utoaji wa boti za  uvuvi, vizimba na kuwezesha kilimo cha zao la mwani.

Naye Mkurugenzi Mkuu wa wa Taasisi ya utafiti wa uvuvi nchini (TAFIRI)Dkt. Ismael Kimirei amesema taasisi hiyo itawasaidia wavumbuzi na watafiti  kwa kuyachukua matokeo  yanutafiti na kuyawekea msingi ili yawe na tija iliyokusudiwa.

Maadhimisho ya wiki ya bahari yanafanyika katika Hoteli ya Ramada Jijini Dar es Salaam kwa muda wa siku tano kuanzia leo Februari 24  hadi 27  mwaka 2025  na yanahusisha wadau   kutoka mataifa mbalimbali Duniani.

Hakuna maoni