Zinazobamba

Madrasa zetu haziko salama, Sheikh Masoud

 



 

Mnamo tarehe 02/02/2024 Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania iliamua kuifunga Madrasa ya Al Habash iliyokuwa maeneo ya Sogea Mbele na Nkuhungu, Dodoma katikati mwa Tanzania kwa tuhuma za kutoa huduma ya elimu katika mazingira hatarishi. Madrasa hiyo ilikuwa na jumla ya wanafunzi wa kike takribani 132 wenye umri wa kati ya miaka 13 hadi 20 katika maeneo yote mawili, wanafunzi hao walikuwa wanatoka maeneo tofauti hususan ndani ya mkoa wa Dodoma.

MAONI:

Tunalaani vikali uamuzi huu usiokubalika wa serikali wa kuifunga madrasa ya Al-Habash bila sababu za msingi. Inaonekana kuwa serikali ilichukua hatua kama sehemu ya muendelezo wa kampeni ya kimataifa dhidi ya Uislamu. Sababu zilizotajwa hazina mashiko kwa serikali kufikia uamuzi huo. Wakati hayo yakijiri, siku chache baadae, tarehe 06/02/2024 serikali iliuvunja msikiti wa wanafunzi katika shule ya sekondari ya Tawalanda iliyopo Bagamoyo mkoani Pwani.

Kampeni ya Kibepari kimataifa ya chuki dhidi ya Uislamu ambayo inasukumwa hasa na Marekani inatumia visingizio mbalimbali kudhibiti, kuingilia kati na kufunga vyanzo vya elimu ya Kiislamu. Hili linafanyika katika ulimwengu wote wa Kiislamu katika zikilengwa Madrasa zenye mfumo wa kiasilia, vyuo vya kati au vyuo vikuu vya Kiislamu.

Ndani ya mwaka 2015 takriban wanafunzi 147 katika Wilaya ya Hai, Kaskazini mwa Tanzania waliokuwa wakisoma katika Madrasa ya misikiti mitatu: Masjid Bilal (Kibaoni), Masjid Othman (Uzunguni) na Masjid kwa Kiriwe waliwekwa kizuizini na vyombo vya dola. (Mtanzania 2 Aprili 2015). Pia katika mwaka huo huo mwalimu wa madrasa, Al-haji Maulana Shiraz (71) wa jumuiya ya Zawiyatul-Qaadiriya katika Wilaya ya Masasi Kusini mwa Tanzania alikamatwa akiwa na wanafunzi 11 tu kwa kisingizio cha vita dhidi ya ugaidi. (Habarileo, 3 Aprili 2015).

Mabepari wakoloni wa kimagharibi walitengeneza propaganda (ya vita vya ugaidi) zinazosababisha mgawanyiko, kuyumbisha kwa watu kijamii na kiuchumi, kueneza chuki, na mara nyingi waendesha mashtaka hushindwa kuleta ushahidi mbele ya mahakama dhidi ya madai ya ugaidi, hata baada ya miaka mingi ya kile kinachoitwa "upelelezi".

Zaidi Endelea hapa:HATA MADRASA ZETU HAZIKO SALAMA CHINI YA UBEPARI

 



Hakuna maoni