Zinazobamba

Mufti Zubeir alimwa barua ya wazi na waislam, kisa ni Bakwata kukaa kimya katika mambo mazito ya waislam



 


 

BARUA YA WAZI KWA MUFTI WA TANZANIA NA BAKWATA

BISMILLAHI RRAHMANI RRAHIYM

ASALAAM ALAYKUM,

YAH: UKIMYA AMMA KUANGAZIA VISIVYO QADHIA ZA WAISLAMU

Tunaandika waraka huu wa nasaha kwako Mheshimiwa Mufti na Baraza Kuu la Waislamu Tanzania (BAKWATA) kwa kuwa dini ya Uislamu imehimiza kupeana nasaha, kuamrishana mema na kukatazana mabaya. Na asili nasaha hizi na mfano wake hupaswa kupewa Waislamu binafsi, taasisi, jumuiya nk. Bali sisi tunazielekeza kwenu kwa nafasi yenu mbele ya Umma ndani ya Tanzania na Uislamu kwa jumla.

Kwa hakika Ummah wa Waislamu nchini Tanzania unasikitishwa na kuhuzunishwa kutokana na ukimya wenu wa kupita mipaka au kuangazia visivyo katika qadhia kadhaa zinazowasibu Waislamu kitaifa na kimataifa.

Baadhi ya qadhia hizo ni kama hizi zifuatazo:

1. Mauaji ya kijidola bandia cha Israil kwa Waislamu wa Gazza na Palestina kwa jumla:

Dhulma, mateso, ukatili na mauaji ya Israili kwa Waislamu wa Palestina asili yamekuwepo kwa miaka 75, lakini yameshitadi zaidi katika hali isiyoelezeka baada ya tukio la mujahidina wa Hamas wanaopigana kujihami (Jihadi diffai) kuingia ndani ya Israil. Mheshimiwa Mufti na BAKWATA kwa kuweka kwenu kumbukumbu sawa, qadhia ya Palestina ina mafungamano ya moja kwa moja kwanza na aqiida ya Kiislamu. Masjid Aqswa ndio qibla cha mwanzo cha Waislamu, kituo cha Safari ya Miujiza ya Mtume SAAW (Israi na Miiraj) na taadhima ya eneo hilo kwani ni sehemu ya eneo la Biladu Shaam. Bali fiqhi ya Kiislamu inalihesabu eneo hilo ni eneo la Umma baada ya kufanyiwa fat-hi na Khalifah Umar Al-Khattab mwaka 17 Hijria/ 638 Miladi. Mauaji haya ya karibu ya Israili yanayoambatana na Waislamu wa Palestina kuzuiliwa kila kitu kuanzia maji, chakula, matibabu nk. yamekuwa yakiendelea mfululizo kwa karibu miezi minne sasa huku sehemu kubwa ya dunia kuanzia baadhi ya nchi, wanaharakati, wanaopenda haki, utu na uadilifu Waislamu na wasiokuwa Waislamu wamekuwa wakipaza sauti zao kupinga, kulaani, kufedhehi dhulma, uharamia na ukatili unaotendwa na kijidola cha Israili. Kwa hapa Tanzania tumeona hata baadhi ya wanasiasa wasiokuwa Waislamu nao wakisimama kidete dhidi ya mauaji hayo. Aidha, baadhi ya Waislamu nchini kwa kujua ufaradhi wa kujihusisha na qadhia za Umma na kutambua Ummah wetu ni Ummah mmoja wamekuwa wakipaza sauti zao kupitia vyombo vya habari, mihadhara, makongamano, mikusanyiko ya nje ( picketing) na hata waliodiriki kutaka kufanya maandamano lakini hawakufanikiwa kwa sababu nje ya uwezo wao. Wakati jitihada hizo zote za ndani na nje zikijiri kulaani dhulma na ukatili wa Israili Mheshimiwa Mufti na BAKWATA kwa masikitiko makubwa mko kimya kana kwamba hakuna kinachoendelea.

Zaidi endelea kwa kubofya hapa....BARUA YA WAZI KWA MUFTI WA TANZANIA NA BAKWATA

 


Hakuna maoni