TASAC,NBS ZAZINDUA RIPOTI YA KWANZA YA SENSA YA VYOMBO VIDOGO VYA USAFIRI MAJINI
Naibu Waziri
wa Ujenzi na Uchukuzi (Sekta ya Uchukuzi) Atupele Mwakibete akizungumza wakati wa uzinduzi wa Ripoti ya
Sensa ya Vyombo Vidogo vya Usafiri Majini katika eneo la Tanzania Bara,
2021.
Shirika la Uwakala wa Meli nchini (TASAC) kwa
kushirikiana na ofisi ya Takwimu ya
Taifa (NBS) limezindua ripoti ya sensa ya vyombo vidogo vya usafiri Majini
ambayo ni ya kwanza kuwahi kufanyika Nchini Tanzania,pamoja na Nchi za Afrika Mashariki na kanda wa Nchi za
Kusini mwa Africa (SADC ).
Akizungumza Wakati wa uzinduzi wa ripoti hiyo Julai 11,2023 Jijini Dar es salaam Naibu Waziri wa Ujenzi na
Uchukuzi anayesimamia Sekta ya Uchukuzi Atupele Mwakibete amebainisha kuwa ripoti hiyo itasaidia kuboresha
sera,kubainisha fursa zilizopo katika kukuza uchumi wa Taifa na watu wake
kupitia uchumi wa bluu.
"kwa mujibu wa taarifa ya sensa jumla ya idadi ya vyombo vidogo vya majini
ni 52,189, pia kuna jumla ya mialo 885,idadi ya vyombo vidogo vya majini vyenye
urefu wa mita nne au zaidi kwenye maeneo ya maji ni 45,976,kati ya hivyo
Asilimia 53.65% vipo Ziwa Victoria, 13.41% vipo Bahari ya Hindi,10.28% vipo
Ziwa Tanganyika,7.65 vipo Ziwa Nyasa na Asilimia 15.1% vipo katika maeneo
mengine ya maziwa na mabwawa nchini" Amesema Mwakibete .
Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania (TASAC)
Kaimu Mkeyenge amesema wakati wa uandaaji wa sensa hiyo wameshirikiana na Ofisi
ya Taifa ya Takwimu (NBS),Wizara ya ujenzi na uchukuzi,TAMISEMI , Wizara ya
Mifugo na Uvuvi pamoja na wadau mbalimbali wa sekta ya Uchukuzi.
“Baada ya kukamilika kwa sensa hii,tumeweza kuunda kanzi data maalumu
inayorahisisha kuvitambua vyombo hivyo,wamiliki na maeneo vilipo na kurahisisha
utambuzi wa vyombo na hali yake na endapo kikitapata majanga kuweza kukifikia
kwa haraka na kutambua ni chombo kipi kimehusika kwenye ajali au changamoto
yoyote majini”Amesema Mkurugenzi Mkuu huyo wa TASAC Kaim Mkeyenge
Hata hivyo Ofisi ya Taifa ya Takwimu
imesema ni mara ya kwanza NBS imeshiriki katika sensa ya vyombo vya majini
hivyo wameipongeza TASAC kwa hatua hiyo na kuongeza kuwa kanzi data iliyoundwa
itasaidia sana Wafanyabiashara,wadadisi na watafiti mbalimbali kufanyakazi yao
kwa urahisi zaidi.
Hakuna maoni
Chapisha Maoni