Zinazobamba

RAIS WA HUNGARY KATALIN VOVAK ANATARAJIWA KUWASILI NCHINI TANZANIA KWA ZIARA YA KIKAZI

Waziri wa  Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Dkt Stergomena  Tax

Na Mussa Augustine

Rais wa Hungary Katalin  Novak  anatarajiwa Kuwasili leo  na kufanya ziara yake  Nchini Tanzania kuanzia  July 17 hadi  20 ,2023   ziara hiyo ikiwa ni matokeo ya jitihada  ya Rais Dk Samia Suluhu Hassan  za Kuimarisha uhusiano wa kidiplomasia na Mataifa mengine.

Hayo yamesemwa  leo  Julai 17 ,2023 na  Waziri wa  Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Dkt Stergomena   Tax wakati akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es salaam nakubainisha kuwa kufanyika kwa ziara hiyo ni moja ya jitihada za  Rais  Dkt Samia Suluhu  Hassan za  kuimarisha uhusiano wa kimataifa na  kikanda.

Aidha  Waziri Tax amesema  ushirikiano uliopo kati ya Tanzania na Hungary ni kuinua sekta ya Elimu kwa kutoa nafasi za mafunzo  mbalimbali katika nyanja mbalimbali hususania katika sayansi na Teknolojia.

“Ujio wa  rasi wa Hungary hapa nchini utaimarisha mashirikiano katika sekta mbalimbaliu ikiwemo sekta muhimu ya elimu,lakini pia tutajadiliana katika maeneo mengine ya uwekezaji” amesema Waziri Tax

Waziri wa  Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Dkt Stergomena  Tax

Kwa upande wake Kamishna wa kitengo cha Fedha za Nje kutoka Wizara ya fedha Rished Bade amesema katika ziara hiyo ya  Rais Katalini  watajadili juu ya uwekezaji wa kilimo,utangazaji,na uzalishaji wa bidhaa mbalimbali ili kuendelea kuimarisha uhusiano kati ya mataifa hayo mawili.

 Mkurugenzi wa kitengo cha habari wizara ya mambo ya nje na ushirikiano wa Afrika Mashariki  Balozi Mindi Kasiga amesema ziara  hiyo  imekuja kutokana na sera mpya  nchini Hungary Kwa nchi za Afrika inayolenga Kuimarisha ushirikiano wa kiuchumi ambao ulianza kutekelezwa  na Taifa hilo miaka michache iliyopita huku akibainisha kuwa uhusiano wa Tanzania  na Hungary ni mzuri tangu enzi za muungano wa Sovieti na kupitia ziara hiyo uhusiano utaimarika .

Mkurugenzi wa kitengo cha habari wizara ya mambo ya nje na ushirikiano wa Afrika Mashariki  Balozi Mindi Kasiga


Hakuna maoni