Zinazobamba

JAJI MTUNGI ­:VYAMA VYA SIASA ZINGATIENI MAELEKEZO YA KISHERIA YANAYOTAKIWA KUFUATWA.

Na Mussa Augustine.

Msajili wa Vyama Vya saiasa Nchini Jaji Francis Mutungi  amevitaka Vyama vya siasa kuzingatia maelekezo ya kesheria yanayotakiwa kufanyiwa marekebisho ili kuvifanya vyama hivyo kutekeleza majukumu yake kwa mujibu wa Sheria.

Agizo hilo amelitoa leo Jinini Dar es salaam wakati akifungua semina ya siku mbili ya viongozi wa vyama vya siasa Nchini,ambapo amesema kuwa Ofisi yake imekua ikiendesha zoezi la kuvihakiki vyama hivyo Kila mwaka ili kujiridhisha kama vinaendesha majukumu yake ya kitaasisi kwa kukidhi matakwa ya kisheria.

"Kabla ya kufanya uhakiki wa vyama hivi vya siasa kwa mwaka huu ,leo tunatoa semina Kwa viongozi wa vyama vya siasa kabla ya kufanya  usajili wa vyama kumi na nane(18) vingine ambavyo  vimeomba kusajiliwa,tukimaliza zoezi hili tunafanya zoezi la uhakiki wa vyama hivyo ili kubaini mapungufu ya kisheria yaliyopo nakuvipa muda wa kuondoa kasoro hizo" amesema Jaji Mutungi

Aidha ameongeza kuwa Vyama Vya Siasa vimekua vikipata hati chafu kufuatia ripoti ya Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa hesabu za Serikali(CAG) kutokana na kushindwa kutunza vizuri kumbukumbu za matumizi ya fedha ndani ya taasisi hizo hivyo kupitia uhakiki huo umelenga kuvifanya vijiendeshe kama taasisi za umma Kwa kuzingatia utunzaji mzuri wa kumbukumbu za matumizi ya fedha.

Kwa upande wake Mwenyekiti Taifa wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania( TCD) Profesa Ibrahim Lipumba amesema kuwa Sheria ya vyama vya siasa imetoa maelekezo ya kuhakikiwa Kila mwaka ili kuangalia mambo mbalimbali ikiwemo rejista ya wananchama,ripoti ya fedha pamoja na Usajili wa bodi ya wadhamini ya chama,hivyo lengo kubwa ni kuvisaidia vyama vya siasa kutekeleza wajibu wake kwa kufuata Sheria.

"Semina hii niya kikazi ,kwani imetukutanisha hapa ili kukumbushana mambo ya Msingi ya kusimamia katika taasisi zetu za vyama vya siasa,amesisitiza  Profesa Lipumba ambaye pia ni mwenyekiti Taifa wa Chama Cha Wananchi ( CUF

Nae mwenyekiti Taifa wa Chama Cha Alliance for Democratic Change( ADC) Hamad Rashid amebainisha kuwa vyama vya siasa vimekua vikipata hati chafu kutokana na kukosa elimu ya namna ya kutunza kumbukumbu za matumizi ya fedha hivyo kupitia semina  hiyo ambayo inatolewa na ofisi ya Msajiri wa Vyama vya siasa itasaidia kuondokana na hati chafu za CAG.

Hata hivyo Naibu Katibu Mkuu CCM Bara  Annamringi Macha amesema  kwamba  vyama vya siasa vipo kwa ajili ya kufanya kazi za maslahi ya Taifa ,hivyo Nia ya msajili wa vyama vya siasa kuvihakiki ni kuvifanya vikidhi matakwa ya kisheria huku akisisitiza kuwa CCM kimekua makini katika utunzaji wa ripoti za matumizi ya fedha ndiyo maana muda mrefu hakijata hati chafu kutoka Kwa CAG.

 

Hakuna maoni