Zinazobamba

WANANCHI KATA YA MZIMUNI WAMPA KONGOLE DIWANI WAO KWA KUWALETEA MAENDELEO.

 

                      Diwani   Manifred Lyoto

Na Mussa Augustine,

Baadhi ya Wananchi wa Kata ya Mzimuni Manispaa ya Kinondoni Wamesema kuwa wanaridhishwa na Utendaji kazi unaofanywa na Diwani wa Kata hiyo (CCM) Manifred Lyoto kwa kuwa kuwaletea maendeleo katika sekta mbalimbali ikiwemo Sekta ya Afya,Elimu,Michezo na Miundombinu ya Barabara na Maji.

Pongezi hizo wamezitoa Juni 27 ,2023 wakati wakizungumza na waandishi wa habari waliotembelea kata hiyo kwa ajili ya kuangalia utekelezaji wa Ilani ya Chama cha Mapinduzi,ambapo kwa nyakati tofauti wananchi hao wamebainisha kuwa kwa sasa kata hiyo imepiga hatua kubwa kimaendeleo.

Mmoja wa Wananchi hao anayefahamika kwa jina la Abdalah Kitumbi Mkazi wa Mtaa wa Mtambani amesema kuwa Diwani huyo ni Kiongozi wa Kuigwa kwani ameboresha sekta ya Elimu kwa kuhakikisha amejenga Uzio wa Shule ya Sekondari na Msingi Mzimuni ,ameweka Miundombinu ya kuwezesha Wanafuzni kupata chakula Shuleni,ameajiri walimu wa masomo ya sayansi hatua ambayo imechangia kuongezeka kwa ufaulu wa wanafunzi.

              Picha ya Masufuria ya Kupikia Chakula 

“Wazazi wanatoa elfu moja tu ya chakula kwa watoto wao ,Miundombinu mingine yote kama vile Jiko,Masufuria,Kontena la kuhifadhia chakula vyote amechangia Diwani kupitia fedha zake mwenyewe ili kuwapunguzia mzigo wa michango wananchi wa Mzimuni,kwakweli amekuwa akijitoa sana kutatua kero za wananchi”amesema Kitumbi.                                                             Picha ya Kontena la kuhifadhai Chakula 

   Picha ya Uzio wa sule katika shule ya Msingi na Sekondari Mzimuni

Nae Irine Mwakingila Mkazi wa Mtaa wa Mwanansari amesema kuwa  Diwani huyo umesaidia kuboresha huduma za afya katika Zahanati ya Mzimuni kutokana na kuoneza watumishi wengine wa afya kwenye Zahanati hiyo ili kuhudumia wakazi wa maeneo hayo na kata jirani.

Ameendelea kusema kuwa Diwani huyo ameanzisha Taasisi ya kutoa Mikopo isiyokua na riba kwa Makundi ya Wajasiliamari  ili kuwawezesha kujikwamua kiuchumi,ambapo Taasisi hiyo iitwayo “Lyoto Foundation” itaanza kutoa mikopo kuanzia Mwezi Julai mwaka huu.

Pia Kassim Kinguyu Mkazi wa Mtaa wa Mtambani amesema kuwa Sekta ya Michezo imepewa kipaumbele kwani tayari baadhi ya timu za Vijana zimepatiwa vitendea kazi vya Michezo ikiwemo Jezi na Mipira,nakwamaba Diwani huyo yupo katika Mazungumzo na wataalamu wa Soka kutoka Mataifa ya Nje kwa ajili ya kuwapeleka vijana wenye vipaji kufanyiwa majaribio ya kucheza soka la Kimataifa.

Hata hivyo kwa upande wake Diwani wa kata ya Mzimuni Manifred Lyoto amesema kuwa ameamua kujitoa kuwasaidia Wananchi wa Kata hiyo kutokana nakwamba Serikali haiwezi kufanya mambo yote kwa wakati Mmoja kwasababu inatekeleza Miradi mingi ambayo inahitaji fedha nyingi.

“Serikali ina mambo mengi yakufanya ,ina miradi mikubwa inayohitaji fedha,hivyo sisi kama wawakilishi wa wananchi kama tunaweza kusaidia kupitia vyanzo vyetu vya binafsi vya Mapato au kutafuta wadau wa kusaidia haina budi kufanya hivyo ili kuinga mkono serikali katika kuwaletea Wananchi Maendeleo “amesema Diwani Lyoto

Nakuongeza kuwa,”Nawaomba Wananchi wa Mzimuni wawe na mwamko mkubwa wa kupeleka watoto wao shuleni kwani tumetatua changamoto zilizokuwepo,tushirikiane kwa pamoja kuleta maendeleo kwenye kata yetu ,siokwamba tusubiri mpaka serikali ifanye”amesema

Kuhusu utoaji wa Mikopo kupitia taasisi ya” Lyoto Foundation” Diwani huyo amesema kuwa wanatarajia kuanza kutoa mikopo hiyo mwezi Julai Mwaka huu ili kuwasaidia Wananchi wa kata hiyo wanaotaka kufanya ujasiliamari kwa lengo la kujikwamua kiuchumi,

Hakuna maoni