Zinazobamba

DC KOMBA AWAOMBA WANANCHI WA GOBA KUJITOKEZA KWA WINGI KUCHANGIA DAMU KWA HIARI

Mkuu wa Wilaya ya Ubungo Hashimu Abdalah Komba

NA Mussa Augustine.

Mkuu wa Wilaya ya Ubungo Hashimu Abdalah Komba amewaomba Wananchi wa Kata ya Goba Wilayani humo kujitokeza kwa wingi katika zoezi la kuchangia Damu kwa hiari litakalofanyika katika Senta ya Goba Juni 24 Mwaka huu.

DC Komba ametoa rai hiyo wakati akizungumza na waratibu wa Kongamanohilo kutoka Taasisi ya Hananja Compasion Foundation pamoja na Shirika la Misaada lakimataifa la Marekani USID kupitia Mradi wake wa “Afya yangu”(Jhpiego USAID) walipo mtembelea ofisini kwake kwa ajili ya kumpatia taarifa ya hatua ya maandalizi ya zoezi hilo.

Aidha amesema kwamba Wananchi wengi wanapoteza maisha kutokana na kukosa damu hivyo elimu inapaswa kuendelea kutolewa ili jamii iwe na utamaduni wakujitoa kwa ajili ya kuchangia Damu kwa hiari ili kuwezesha kuwepo na Damu ya kutosha Mahospitalini.

“Damu ndio Maisha,Damu haina Mbadala wake,haiuzwi hivyo mimi na wewe(Mwananchi)tunataka Damu ,ni wakati sasa wa kuwa na tabia ya kuchangia Damu kwa hiari ili kuokoa Maisha ya Dungu zetu pamoja na Wengine wanaopatwa na matatizo mbalimbali ikiwemo ajali”amesema DC Komba

Nakuongeza kuwa”Wakina Mama wajawazito wanapoteza maisha wakati wa kujifungua kutokana na kukosa Damu,nawaomba sana Wananchi wa Goba na maeneo mengine wajitokeze jumamosi ya tarehe 24 mwezi huu wa sita wachangie Damu kwa hiari ili tuwe na akiba ya Damu ya kutosha Mahospitalini.

Mratibu wa Damu Salaama  Manispaa ya Ubungo  Analimi Machalo

Kwa upande wake Mratibu wa Damu Salaama  Manispaa ya Ubungo  Analimi Machalo amebainisha kuwa Wilaya hiyuo imejiwekea lengola kukusanya Uniti 311 kwa mwezi,huku kwa mwaka imepanga kukusanya Uniti 3731 za Damu,nakwamba hadi sasa Wilaya hiyo imekusanya Uniti 1505 sawa na asilimia 40.

Aidha ameongeza kuwa siku ya zoezi hilo litakalofanyika Goba wanatarajia kukusanya Uniti 300 za Damu hivyo amewaasa Wananchi kujitokeza kwa wingi ili kuchangia Damu kwa hiari nakuwezesha kufikia malengo waliojiwekea nakuwa na Damu ya kutosha Mahospitalini.

Hakuna maoni