MSAMA PROMOTIONS YAWATAMBULISHA BAADHI YA WAIMBAJI WA NYIMBO ZA INJILI TAMASHA LA PASAKA
Na Mussa
Augustine.
Kampuni ya
Msama Promotion ambayo imeandaa tamasha kubwa la Pasaka imetaja baadhi ya Waimbaji wa Nyimbo za Injili
ambao wamethibitisha kuwepo katika
tamasha hilo litakalofanyika April .9. 2023, katika Uwanja wa Uhuru Jijini Dar
es salaam.
Akizungumza
na Waandishi wa habari Februari 24.2023 jijini Dar es salaam, Mkurugenzi wa
kampumi hiyo Alex Msama amesema kwamba tamasha la awamu hii litakua la aina
yake kwani waimbaji nguli wa nyimbo za injili kutoka ndani na nje ya Tanzania wanatarajiwa
kushiriki.
Mkurugenzi
huyo pia amesema kwamba Tamasha hilo linaenda samabamba na sherehe za miaka
miwili ya Rais Dkt Samia Suluhu Hassan tangu aingie madarakani baada ya
mtangulizi wake Hayati Dkt Jonh Magufuli kufariki dunia.
“Siku ya
Tamasha la Pasaka tutaliombea Taifa letu
na Viongozi akiwemo Rais Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kazi kubwa na nzuri anayoifanya
ya kuwatumikia Watanzania na kuliletea
Taifa letu Maendeleo,tumekuwa tukishuhudia majanga mbalimbali yanajitokeza kwa
nchi zingine hivyo kupitia tamasha hili tutafanya maombi ya kulinusuru Taifa letu
na majanga mbalimbali kama vile Vita,Ukame , Njaa na Mafuriko”amesema
Msama amesema
Kwamba Tayari Baadhi ya Waimbaji Nguli wa Nyimbo za Injili kutoka Hapa Nchini
na Nje ya Nchi wamethibitisha kushiriki katika Tamasha hilo lianalotarajiwa
kuwa na mambo mengi mbalimbali yatakayofanyika huku akiwaomba watanzania
kujitokeza kwa wingi kushuhudia na kuimba kwa pamoja kwa ajili ya kumsifu
Mungu.
“Waimbaji waliothibitisha
kushiriki Tamasha hili ni Tumaini
Akilimari kutoka Kenya,Joshua Ngoma kutoka Rwanda,Upendo Nkone ,Ambwene Mwasongwe hawa nikutoka Tanzania,pamoja na Mwimbaji
Masi Masilia kutoka nchini Kongo ambaye anakuja kwa mara ya kwanza hapa nchini hivyo Watanzania wajitokeze kwa wingi kushuhudia tamasha hili” amesema
kwa bashasha kubwa.
Nkuongeza
kuwa “bado tunaendelea kufanya mazungumzo na waimbaji wengine kutoka Mataifa
mbalimbali ikiwemo Afrika Kusini,Uingereza na Marekani ili washiriki katika Tamasha hili ,hivyo wale
watakaokubali kushiriki tutaendelea kuwafahamisha Watanzania,lakini kuna baadhi
ya kwaya zimekubali kushirikiana nasi ikiwemo Zabron Singers.
Hakuna maoni
Chapisha Maoni