Zinazobamba

TCCIA Yaishauri TRA Kuwa na Utamaduni wa Kukutana na Wafanyabiashara Kujadili Kodi


Na Mussa Augustine

 Chama Cha Wafanyabiashara wenye Viwanda na Kilimo (TCCIA) imeiomba serikali kupitia Mamlaka ya Mapato Nchini ( TRA) kuweka utamaduni wa kukutana na wafanyabiashara kujadili namna ya kuweka mifuno mizuri ya ukusanyaji wa kodi stahiki hali itakayosaidia wafanyabiashara hao kulipa kodi kwa hiari nakwa wakati.

 Rai hiyo imetolewa leo na Mkurugenzi Mkuu wa TCCIA Nebart Mwapwele wakati wa majadiliano ya mradi wa Husisha kwa maendeleo Endelevu unaotekelezwa na TCCIA kwa kushirikiana na TRIAS, ambapo majadiliano hayo yamelenga kuondoa changamoto zinazowakabili wafanyabiashara wakati wa kulipa kodi.

 Aidha amesema kuwepo kwa majadiliano ya mara kwa mara kati ya TRA na wafanyabiashara inasaidia kutoa elimu ya kuboresha mifumo ya upimaji kodi kwa hiari nakuondoa njia ya matumizi ya nguvu.

 Mjadala huo umewakutanisha wadau mbalimbali kutoka makampuni 50 ya wafanyabiashara,sekta za huduma kama vile Watunga sera za kodi,wasimamizi wa kodi,wadau wa maendeleo ,wataalamu wa kodi , Wanataaluma , Mashirika ya utafiti, wadau kutoka Wizara ya fedha na mipango ili kujadili kwa pamoja changamoto zinazowakabili wafanyabiashara nakushindwa kulipa kodi kwa wakati.

 "Mjadala huu unahisi masuala ya kodi,hatuna washiriki wa sekta mbalimbali ikiwemo TRA na taasisi ambazo zinawasimamia wafanyabaishara ,lengo ni kumpa mfanyabiashara elimu kuhusu masuala ya kodi ili alipe kodi stahiki na kwa hiari" alisema 

 Naye Makamu Rais Biashara TCCIA Dkt Kulwa Meshack amesema kwamba wamekuwa wakihamasisha wanachama wa TCCIA walipe kodi kama wajibu wao kwa mujibu wa sheria ili kuondoa misuguano kati ya TRA na Wafanyabiashara hao.

 Amesema kwamba TCCIA imekua ikishirikiana Vizuri na TRA kupitia kitengo cha huduma kwa mlipa kodi  kuelimisha wanachama kuhusu elimu ya kodi nakuondoa mifumo mibovu ya ulipaji kodi inayowaumiza wanachama.

 " Hakuna sababu yakusema tumekadiria vibaya na TRA wametusikia hivyo malalamiko ya kutozwa kodi isiyo stahiki yatakwisha kwasababu tunaendelea kujadiliana na TRA kuangalia mifumo yote mibovu ya kulipia kodi  nakuweza  mifumo mizuri " amesema Dkt Meshack

 Kwa upande wake Meneja Elimu kwa Mlipa Kodi kutoka TRA JUlius Mjenga amesema wamesikiliza maoni na mapendekezo ya wadau hao nakwamba TRA inaendelea kuyafanyia kazi maeneo ambayo bado yanaleta ukakasi wa kulipa kodi kwa wafanyabiashara hao.

 


Hakuna maoni